Header Ads

MAKAMU WA RAIS MGENI RASMI KATIKA KILELE CHA KIZIMKAZI DAY


post-feature-image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka shira kwenye kalmati kwenye kilele cha sherehe za Siku ya Kizimkazi (Kizimkazi Day) ambapo vyakula vya asili huliwa.
 Vijana wa Kiume wakishindana kukuna nazi ikiwa sehemu ya mashindano ya Siku ya Kizimkazi (Kizimkazi Day).
 Wakina Mama wakishindana kufunga kamba kwenye kilele cha sherehe za Kizimkazi.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakazi wa kijiji cha Kizimkazi Mkunguni kwenye kilele cha Sherehe za Siku ya Kizimkazi ambapo wanakijiji hutumia siku hiyo maalum kujadiliana mambo ya maendeleo na kushiriki michezo mbalimbali pamoja na kula vyakula vya asili pamoja.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi  kutoka kwa wakina mama wa kijiji cha Kizimkazi Mkunguni kwenye kilele cha sherehe za Siku ya Kizimkazi
 5. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Ndugu Idrisa Kitwana wakati wa kilele cha sherehe za siku ya Kimkazi (Kizimkaziday) kwenye kijiji cha Kizimkazi Mkunguni. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Powered by Blogger.