Watuhumiwa dawa za kulevya wazidi kubanwa
WAZIRI
 Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa, Kassim Majaliwa 
amemtaka Mkuu wa Magereza mkoa wa Lindi, kuhakikisha hakuna mtuhumiwa wa
 dawa za kulevya atakayetoweka katika gereza la mkoa huo.
Amesema
 kuna watuhumiwa wa dawa za kulevya ambao wanahifadhiwa katika gereza la
 mkoa wa Lindi hivyo ni vema akajiridhisha kama ulinzi na usalama wa 
watuhumiwa hao umeimarishwa.Hata hivyo, Waziri Mkuu, Majaliwa amemtaka 
mkuu wa gereza hilo kuwa makini na baadhi ya zabuni wanazozitoa kutoka 
nje na kuhakikisha ulinzi unaimarisha wakati wote gerezani hapo.
Waziri
 Mkuu, Majaliwa ameyasema hayo jana (10 Aprili, 2016)  wilayani Ruangwa 
wakati akipokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Lindi iliyowasilishwa 
kwake na Mkuu wa mkoa huo, Godfrey Zambi.“Mkuu wa Magereza wa mkoa 
atembee gereza ambalo wanashikiliwa watuhumiwa wa dawa za kulevya na 
aangalie mradi unaolenga kupeleka maji gerezani hapo kama ni kweli au 
njia…,” amesema Waziri Mkuu, Majaliwa.
Aidha,
 Waziri Mkuu, Majaliwa amemtaka mkuu huyo wa Magereza kujiridhisha kama 
ulinzi na usalama wao umeimarishwa na kuhakikisha hakuna mtuhumiwa 
anayetoweka.Awali akisoma taarifa kwa Waziri Mkuu,  mkuu wa mkoa wa 
Lindi, Zambi amesema matumizi ya dawa za kulevya hususan kwa vijana ni 
miongoni mwa changamoto zinazoukabili mkoa huu ambapo wilaya ya Kilwa 
inaongoza kwa kuwa na waathirika wengi.
Amesema
 matumizi ya dawa hizo yanasababisha kupunguza kwa nguvu kazi kwani 
watumiaji wengi ni vijana, hivyo alitoa wito kwa wananchi kushirikiana 
na serikali katika kupiga vita matumizi ya dawa hizo kwa kuwafichua 
wauzaji na watumiaji.
Imetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu

No comments:
Post a Comment