Header Ads

WANAFUNZI 538 WATUNUKIWA VYETI VYAO KATIKA MAHAFALI YA NANE YA CHUO CHA TRA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.

WANAFUNZI 538 wa chuo cha Mamlaka ya Mapato (TRA) wametunukiwa vyeti vyao leo katika mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.

Pia wahitimu hao wameaswa kuwa waadilifu katika kazi zao kwani taaluma yao ni ukusanyaji wa mapato ya sehemu zao za kazi.

Wameaswa hayo na  Naibu waziri wa Fedha na Mipamgo, Ashatu Kijaji wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa mahafali ya nane ya chuo cha Mamlaka ya Mapato (TRA) yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere.

amesema kuwa wahitimu wa chuo hicho wafanye kazi kwa weredi na uaminifu  kwani wasipofanya hiyo hawataweza kufanya kazi hayo vile inavyopaswa.

Chuo cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kitajengwa kingine huko  kibaha mkoani pwani ili kuongeza wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri kwani chuo kilichopo Mwenge kimezungukwa na viwanda.




 Naibu waziri wa Fedha na Mipamgo, Ashatu Kijaji akizumgumza na wahitimu wa chuo cha Mamlaka ya mapato Tanzania TRA leo katika mahafali ya nane ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere leo jijini Dar es Salaam


No comments:

Powered by Blogger.