Header Ads

BENKI YA WANAWAKE YATAKIWA KUWAWEZESHA KIUCHUMI NA KIELIMU WANAWAKE

Na.Catherine Sungura-WAMJW.
 
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu, ameitaka Bodi na Watendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania (TWB), kuhakikisha kuwa inawawezesha wanawake kiuchumi kwa kufikisha huduma hiyo mbali zaidi ili kuifanya benki kuwa kimbilio la wanawake kweli . 
 
Akizungumza katika ziara yake ya mafunzo katika benki hiyo akifuatana na Naibu wake waziri Dakta HAMISI KIGWANGA, Katibu mkuu na watendaji wa Wizara hiyo UMMY alisema wanawake wa Tanzania wanajitoa sana katika kulea familia hivyo wakiwezeshwa watakuwa wamewezesha familia, vijana na Taifa kwa ujumla.
 
Waziri huyo alisema   watendaji wa benki hiyo ya wanapaswa kuweka utaratibu mzuri wa utoaji wa huduma ambazo zitaweka fikra za wanawake pale wanapotaka kuchukua mikopo au kuweka fedha zao katika benki kufikiria kwanza benki ya TWB.
 
“Mimi huwa naona uwezeshaji wa kweli wa wanawake ni kuhakikisha kuwa tunawawezesha kiuchumi na kielimu kwasababu mwanamke atashiriki kulima kupanda lakini ikifika kuvuna tu mazao sio yake hivyo endapo tutapata fedha zinazohusu mfuko wa wanawake Serikalini tutaomba zipitishwe kwenye Benki ya Wanawake na tutakwenda kila Halmashauri kuanzisha saccos za wanawake ili waweze kupata fedha za kukopeshwa na benki ya wanawake,’’alisema Ummy.

No comments:

Powered by Blogger.