Header Ads

UMEME WA MAKAA YA MAWE LAZIMA : Prof. Muhongo

????????????????????????????????????
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akizungumza na baadhi ya watendaji wa Mgodi wa Makaa ya Mawe ya Ngaka mara baada ya kuwasili katika mgodi huo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoa wa Ruvuma. Wengine ni ujumbe aliofuatana nao   pamoja na Mbunge wa Mbinga vijijini, Martin Msuha, Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga, Kamishna Msaidizi wa Madini, anayeshughulikia Leseni John Nayopa, Watendaji toka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC), Ofisi ya Madini Kanda ya Ziwa Nyasa, baadhi ya Maafisa toka Wizara ya Nishati na Madini na EWURA.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo, (kulia) akiwasikiliza wawakilishi wa wananchi wa Kijiji cha Mtundualo, Wilaya ya Mbinga ambao walimwomba waziri asikilize malalamiko yao  ikiwemo kuhusu suala la fidia kupisha mradi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka na ombi la kijiji hicho kupatiwa umeme.  Kwa mujibu wa Meneja wa Tanesco Kanda ya Kusini, Joyce Ngahyoma, amewahakikishia kuwa ifikapo  mwezi Aprili mwaka huu kijiji hicho kitakuwa kimeunganishwa na nishati ya umeme.
????????????????????????????????????
Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga, akijadiliana jambo na baadhi ya Watendaji wa Mgodi wa Ngaka kampuni ya TANCOAL, mara baada ya waziri kukagua shughuli za mgodi huo na kusikia malalamiko ya wananchi kuhusu fidia. Waziri Muhongo amezitaka pande mbili kati ya Kampuni, Halmashauri na wananchi kukutana ili kujadili na kukubaliana kuhusu masuala kadhaa yakiwemo fidia na uhifadhi wa mazingira.

No comments:

Powered by Blogger.