UMEME WA MAKAA YA MAWE LAZIMA : Prof. Muhongo
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akizungumza
na baadhi ya watendaji wa Mgodi wa Makaa ya Mawe ya Ngaka mara baada ya
kuwasili katika mgodi huo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoa wa Ruvuma.
Wengine ni ujumbe aliofuatana nao pamoja na Mbunge wa Mbinga
vijijini, Martin Msuha, Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga, Kamishna
Msaidizi wa Madini, anayeshughulikia Leseni John Nayopa, Watendaji toka
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya Taifa
(NDC), Ofisi ya Madini Kanda ya Ziwa Nyasa, baadhi ya Maafisa toka
Wizara ya Nishati na Madini na EWURA.
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospter Muhongo, (kulia) akiwasikiliza
wawakilishi wa wananchi wa Kijiji cha Mtundualo, Wilaya ya Mbinga ambao
walimwomba waziri asikilize malalamiko yao ikiwemo kuhusu suala la
fidia kupisha mradi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka na ombi la kijiji hicho
kupatiwa umeme. Kwa mujibu wa Meneja wa Tanesco Kanda ya Kusini, Joyce
Ngahyoma, amewahakikishia kuwa ifikapo mwezi Aprili mwaka huu kijiji
hicho kitakuwa kimeunganishwa na nishati ya umeme.
Mkuu
wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga, akijadiliana jambo na baadhi ya
Watendaji wa Mgodi wa Ngaka kampuni ya TANCOAL, mara baada ya waziri
kukagua shughuli za mgodi huo na kusikia malalamiko ya wananchi kuhusu
fidia. Waziri Muhongo amezitaka pande mbili kati ya Kampuni, Halmashauri
na wananchi kukutana ili kujadili na kukubaliana kuhusu masuala kadhaa
yakiwemo fidia na uhifadhi wa mazingira.
No comments:
Post a Comment