MKUU WA WILAYA YA RUANGWA MKOA WA LINDI,MARIAM MTINA ATOA MACHOZI WAKATI WA KUPOKEA MSAADA MASHINE TOKA VODACOM FOUNDATION
 Mkuu 
wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(wasita toka 
kushoto)akimsikiliza kwa umakini Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya
 hiyo, Omary Rajabu(kulia)alipokuwa akiwaelezea baadhi ya wafanyakazi wa
 Vodacom Tanzania,Wauguzi wa hospitali hiyo na wananchi jinsi mashine 
inayofyonza uchafu(Electrical Suction machine) kwa watoto waliozaliwa 
kabla ya wakati”Njiti” Zaidi ya shilingi Milioni 6/- zilitumika katika 
kunua vifaa hivyo na kutolewa msaada na Vodacom Foundation kupitia 
taasisi inayojishughulisha na watoto hao ya Doris Mollel. 
 Mkuu 
wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(wapili toka 
kushoto)pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania, Wauguzi wa 
hospitali hiyo na wananchi wakimsikiliza Mganga Mkuu wa Wilaya ya 
Ruangwa,Dkt Japhet Simeo(kushoto)akiwaelimisha jinsi mashine ya Oxygen 
inavyosaidia watoto waliozaliwa kabla ya wakati”Njiti” kupumua wakati wa
 hafla fupi ya makabidhiano ya msaada wa mashine hizo zilizogharimu 
zaidi ya shilingi milioni 6/- na kukabidhiwa na Vodacom Foundation 
kupitia taasisi inayojishughulisha na watoto hao ya Doris Mollel.
 Mkuu 
wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(katikati)akitoa 
shukurani kwa niaba ya wananchi wake kwa Meneja wa Vodacom 
Foundation,Sandra Oswald na Mwanzilishi wa taasisi ya Doris Mollel 
inayojishughulisha kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya 
wakati”Njiti”,Doris Mollel(kulia)kuhusiana na msaada wa mashine ya 
kupumulia na vifaa mbalimbali uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia 
taasisi ya Doris Mollel vya kuwasaidia watoto hao wanaozaliwa katika 
wilaya hiyo.Vifaaa hivyo viligharimu zaidi ya shilingi milioni 6/-
 Mkuu 
wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,Mariam Mtina(watatu toka 
kushoto)akipokea msaada wa mashine inayofyonza uchafu kwa watoto 
waliozaliwa kabla ya wakati”Njiti”kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo 
toka kwa Meneja wa Vodacom Foundation, Sandra Oswald.Msaada huo 
uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia taasisi ya Doris 
Mollel,Uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 6/-
Baadhi
 ya wakazi wa Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi,wakifurahia msaada wa 
mashine mbalimbali uliotolewa na Vodacom Foundation kupitia taasisi ya 
Doris Mollel inayojishughulisha kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya 
wakati”Njiti”Msaada huo ulikabidhiwa hivi karibuni.





No comments:
Post a Comment