DC KINONDONI KUONGOZA UPIMAJI WA MAGONGWA YA MOYO BURE VIWANJA VYA LEADERS CLUB JIJINI DAR ES SALAAM KESHO KUTWA JANUARY 23,2016
Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), akizungumza katika
mkutano na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dar es Salaam leo asubuhi
wakati akitoa mwito kwa wananchi hasa wa Wilaya ya Kinondoni na maeneo
mengine ya jiji la Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupimwa maradhi ya
moyo bure katiza zoezi litakalofanywa na madaktari kutoka taasisi hiyo
litakalofanyika viwanja vya leaders kesho kutwa January 23, 2015.
Kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo, Salome Kassanga na Kaimu Mkurugenzi
wa Taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi.
Kaimu
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi (kushoto),
akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,
Paul Makonda.
Meneja
wa Taasisi hiyo, Salome Kassanga (kushoto), akimuelekeza jambo DC
Makonda. Katikati ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo wa Taasisi hiyo,
Dk.Peter Kisenge.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
No comments:
Post a Comment