UPDATES KUTOKA DODOMA: RAIS KIKWETE AFUNGA MKUTANO MKUU WA CCM MJINI DODOMA LEO, KUMTAMBULISHA MAGUFULI UWANJA WA JAMHURI JANA


Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama, wakati wa kuufunga Mkutano huo jioni
hii kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM (Dodoma Conveition Centre), uliopo
Mjini Dodoma. CCM wanafanya mkutano mkubwa wa kumtambulisha Mgombea wao
jioni hii kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.


Mwenyekiti
wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akiwatambulisha Mgombea Urais wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli pamoja
na Mgombea Mwenza, Mh. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuufunga
Mkutano huo.

Rais
Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin Mkapa akimkumbatia Dkt. John
Pombe Magufuli wakati akimpongeza kwa ushindi alioupata.

Mgombea Urais wa CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Mzee Pius Msekwa na Mzee Ali Hassan Mwinyi.
No comments:
Post a Comment