Header Ads

MEZ B AFARIKI DUNIA MKOANI DODOMA

Mez BMwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Moses Bushagama ‘Mez B’ amefariki Dunia katika hospitali moja mkoani Dodoma ambako alikuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa mwanamuziki huyo, wamesema kwamba marehemu alikuwa yupo katika hatua za mwanzoni za matibabu ya ugonjwa wa kifua kikuu(T.B)..
Mez B alianza kusikika rasmi miaka ya 2000  akitamba  na vibao  kama vile Kama vipi, Nimekubali na nyinginezo huku akiwa ni mmoja wa memba kutoka katika kundi la Chemba Squad ambalo lilikuwa linaundwa na late Albert Mangwair, Noorah pamoja na Dark Master.
Hata hivyo miaka ya hivi karibuni, Mez B alishindwa kutamba kwa kile alichokitaja kuwa ni kukosa airtime ya kutosha katika redio za hapa nyumbani.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi

No comments:

Powered by Blogger.