Header Ads

Tathmini Ya Programu ya IFAD nchini Tanzania yaonyesha Mafanikio Makubwa

Mkurugenzi wa IFAD, Ofisi huru ya Tathmini, Mr Oscar Garcia akitoa ripoti ya tathmini ya programu ya IFAD nchini Tanzania jinsi ilivyoweza kuonyesha mafanikio makubwa wakati wa warsha ya siku moja iliyofanyika Januari 29, 2014 jijini Dar katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere.
 Waziri wa Kilim, Chakula na Ushirika Tanzania Bara, Mh Steven Wassira akisoma hotuba fupi wakati wa warsha ya siku moja iliyolenga kuonyesha mafanikio ya programu ya IFAD nchini Tanzania, warsha iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere Januari 29, 2014 jijini Dar.
Waziri wa Kilimo na Maliasili wa Zanzibar, Mh Sira Ubwa Mamboya akizungumza wakati wa warsha ya siku moja iliyofanyika Januari 29, 2014 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwl Nyerere wakati wa kuwasilisha ripoti ya tathmini ya programu ya IFAD nchini Tanzania.
Nadine Gbossa, Mkuu wa Ofisi ya Kanda ya IFAD Nairobi akizungumzia tathmini ya mafanikio ya programu ya IFAD nchini Tanzania katika warsha ya siku moja iliyofanyika Januari 29 2014 jijini Dar Es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl Nyerere.

No comments:

Powered by Blogger.