PICHA:WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII LAZARO NYALANDU AZIDI KUFANYA MAKUBWA MALIASILI NA UTALII

Meneja
wa Mbuga ya wanyama ya Selous, Benson Kibonde akimpatia maelezo kuhusu
masalia ya injini ya mvuke iliyoachwa na Wajerumani, kwa Waziri wa
Maliasili na Utalii Lazao Nyalandu (kushoto), waziri huyo alipofika
katika mbuga hiyo, kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kupokeavifaa vya
kukabiliana na ujangili vilivyotolewa na serikali za Marekani na
Ujerumani kwa ajili ya Mbuga ya Selous leo
Maelezo kuhusu masalia hayo ya injini hiyo ya moshi iliyoachwa na wajerumani Benson Kibonge 
Waziri
Nyalandu akitembela maeneo mbalimbali ya mbuga hiyo ya Selous kabla ya
kukabidhiwa vifaa hivyo ya kukabiliana na ujangili katika mbuga ya
wanyama ya Selous leo. anayemuongoza na Meneja wa mbuga hiyo
Waziri Nyalandu akisalimiana na Ofisa Mawasiliano na Umma wa Ubalozi wa
Marekani nchini Tanzania, David Feloemann, alipowasili kwenye mbuga ya
Selous leo
Mkurugenzi
wa theNkoromo Blog, Bashir Nkoromo, ambaye alialikwa kwenye hafla hiyo,
akitazama mto Ruaha unaopita katika mbuga ya Selous 
Waandishi wa habari wakiwa kwenye hafla hiyo
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza maneno ya
Utangulizi kabla ya kukabidhiwa vifaa vya kukabiliana na ujangili kutoka
na serikali za Marekani na Ujerumani katika hafla hiyo. Kulia ni Balozi
wa Mrekani Mark Childress na waili kulia ni Balozi wa Ujerumani Egon
Kochanke
Balozi
wa Marekani nchini, Mark Childress akizungumza kabla ya kutiliana saini
na Nyalandu mkataba ya kukabidhiana vifaa hivyo. Kushoto ni Balozi wa
Ujerumani Egon Kochanke

Balozi
wa Marekani Mark Childress na Waziri wa Maliasili na Utalii wa
Tanzania, Lazaro Nyalandu wakitiliana saini mkataba wa Marekani kuipa
Tanzania msaada wa mafunzo yakiwemo ya kikomandoo kwa askari wa
wanyamapori na vifaa vya kisasa vya kukabiliana na ujangili katika mbuga
ya wanyamapori ya Selous leo.

Waziri
Nyalandu akibadilishana hati na Balozi wa Marekani, Mark Childress
baada ya kusaini mkataba huo. Kushoto ni Balozi wa Ujerumani Egon
Kochanke
No comments:
Post a Comment