Header Ads

Picha:Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini Jonson Minja amefikishwa Mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa Mashitaka mawili ikiwemo la kuchochea Wafanyabiashara wasilipe kodi ya Serikali.

  Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini, Bw. Jonson Minja aliyevaa koti akisindikizwa katika mahakama ya mkoa wa Dodoma chini ya ulinzi wa askari polisi.
Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini, Bw.  Jonsoni Minja akisomewa mashataka yake katika mahakama ya mkoa wa Dodoma.
Mweyekiti wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini, Bw.  Jonsoni Minja aliyevaa koti huku akiongea na katibu wake Mchungaji Kiondo akisubili kusomewa mashitaka yake mawili likiwemo la kuchochea Wafanyabiashara  wasilipe kodi ya Serikali  katika mahakama ya mkoa wa Dodoma.
----
Na John Banda,Dodoma

MWENYEKITI wa Shirikisho la vyama vya Wafanyabiashara Nchini Jonson Minja  amefikishwa Mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa Mashitaka mawili ikiwemo la kuchochea Wafanyabiashara  wasilipe kodi ya Serikali.

Akisoma Mashitaka hayo Wakili wa Serikali Gogfrey Wambari mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Rebbeka Mbiru alisema mtuhumiwa alitenda makosa hayo tarehe 6 Septemba 2014 alipokuwa katika mkutano na Wafanyabiashara katika ukumbi wa Chuo cha Mipango Dodoma.

No comments:

Powered by Blogger.