Header Ads

RAIS MUGABE AMTIMUA KAZI MAKAMU WAKE


Robert MugabeRais wa Zimbambwe Robert Mugabe amewafukuza kazi mawaziri wake wawili na manaibu waziri wapatao watato, hatua ambayo imemkumba aliyekuwa makamo wake Joyce Mujuru.
Hatua hii ya kuwafuta kazi mawaziri wake inafuatia hali tete ya kisiasa nchini humo na kujiandaa na lolote litakalotokea lakini pia ni kutokana na mafanikio hafiifi ya kiongozi uyo mwenye umri wa miaka 90 endapo atajiuzulu ama kufa.
Mugabe ambaye siku za hivi karibuni ameamua kupumzika katika msimu huu wa sikukuu na kuchagua kwenda katika bara la Asia kupumzika yeye na familia yake.
Joyce Mujuru
Bi.Joyce Mujuru
Wadadisi wa mambo nchini zimbabwe wanasema mafaniko ya Rais uyo hayakutarajiwa na walio wengi, pia anasema hofu ya kupokwa madaraka aliyonayo Rais Mugabe ilimsukuma kumtimua kazi makamu wa Rais wake bi.Joyce Mujuru aliyekuwa akipata umaarufu mkubwa kisiasa nchini mwake.
Mujuru aliingia katika kashfa ya kutaka kumuua Rais lakini pia anashtumiwa kwa kukigawa chama cha ZANUPF na lingine ni kushindwa kwake kufunga mikataba ya kibiashara.
Kufuatia tuhuma hizo nafasi ya Bi.Mujuru ilichukuliwa na waziri Emmerson Mnangagwa ambaye ni mshirika wa miaka mingi wa Rais Mugabe na mmoja kati ya viongozi maarufu sana nchini Zimbabwe.

No comments:

Powered by Blogger.