ESSEBSI ASHINDA UCHAGUZI HURU WA KWANZA WA URAIS TUNISIA
Mwanasiasa mkongwe wa Tunisia ‘Beji Caid Essebsi’ ameshinda
uchaguzi huru wa kwanza wa urais kuwahi kufanyika nchini humo kupitia
tiketi ya chama chake cha Nidaa Tounes tangu vuguvugu la mataifa ya
kiarabu kumuondoa dikteta Zine El-Abidine Ben Ali mwaka 2011.
kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa Jumatatu(Dec.22) na
mamlaka ya uchaguzi, Essebsi Mwenye umri wa miaka 88, aliibuka mshindi
dhidi ya mpinzani wake Moncef Marzouki kwa asilimia 55.68 ya kura kati
ya asilimia 44.32 katika uchaguzi uliomalizika Jumapili(Dec.21) mara
baada ya serikali ya mpito nchini humo kuimarisha Demokrasia kwa kipindi
cha miaka 4 iliyopita.
Wagombea wote walitakiwa wawe watulivu baada ya maandamano
yaliyozuka katika miji kadhaa ya kusini juu ya kurudi kwa vikosi vya
ulinzi vya zamani.
Ushindi huo unaonekana kama kilele cha mageuzi ya kisiasa kwa kuwa nchi hiyo imepitia machafuko kwa takribani miaka 4 iliyopita.
”Nitakuwa Rais kwa ajili ya wananchi wote wa Tunisia’‘, alisema Essebsi katika hotuba fupi aliyokuwa akiitoa kwenye televisheni ya serikali.

No comments:
Post a Comment