Header Ads

ESSEBSI ASHINDA UCHAGUZI HURU WA KWANZA WA URAIS TUNISIA


Pichani ni Rais mpya wa Tunisia Beji Caid Essebsi
Pichani ni Rais mpya wa Tunisia Beji Caid Essebsi
Mwanasiasa mkongwe wa Tunisia ‘Beji Caid Essebsi’ ameshinda uchaguzi huru wa kwanza wa urais kuwahi kufanyika nchini humo kupitia tiketi ya chama chake cha Nidaa Tounes tangu vuguvugu la mataifa ya kiarabu kumuondoa dikteta Zine El-Abidine Ben Ali mwaka 2011.
kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa Jumatatu(Dec.22)  na mamlaka ya uchaguzi, Essebsi Mwenye umri wa miaka 88, aliibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake Moncef Marzouki kwa asilimia 55.68 ya kura kati ya asilimia 44.32 katika uchaguzi uliomalizika  Jumapili(Dec.21) mara baada ya serikali ya mpito nchini humo kuimarisha Demokrasia kwa kipindi cha miaka 4 iliyopita.
Wagombea wote walitakiwa wawe watulivu baada ya maandamano yaliyozuka katika miji kadhaa ya kusini  juu ya kurudi kwa vikosi vya ulinzi vya zamani.
Ushindi huo unaonekana kama kilele cha mageuzi ya kisiasa kwa kuwa nchi hiyo imepitia machafuko kwa takribani miaka 4 iliyopita.
”Nitakuwa Rais kwa ajili ya wananchi wote wa Tunisia’‘, alisema Essebsi katika hotuba fupi aliyokuwa akiitoa kwenye televisheni ya serikali.

No comments:

Powered by Blogger.