Wanafunzi Feza Schools washinda kimataifa 'Genius Olympiad'
Mwanafunzi
wa Shule ya Kimataifa ya Fedha mwaka 11, Khalfan Kikwete (kulia) ambaye
alishinda medali ya dhahabu pamoja na mwenzake Seif Yahya Mhata
wakizungumza na waandishi wa habari.
Mwanafunzi
Veronica Samuel Ndomba akielezea (kulia) katika picha na bendera ya
nchi yake mara baada ya ushindi katika mashindano ya Genius Olympiad
hivi karibuni.
Picha ya Mwanafunzi Prince Mwemezi Muzamil Katunzi aliyoipiga na kushinda katika mashindano ya Genius Olympiad.
Wanafunzi
wa Shule za Feza Tanzania walioshinda mashindano ya taaluma kimataifa
ya 'Genius Olympiad' katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu wao.
Mwanafunzi
Yahya Mhata ambaye kwa pamoja wamebuni mfumo huo, ameuelezea kuwa ni
mzuri na rafiki wa mazingira huku ukiweza kuhifadhi kumbukumbu za
mawasiliano kwa uhakika tofauti na ule wa kadi za makaratasi ambao wengi
hupoteza kadi hizo na kujikuta wakipoteza mawasiliano muhimu.
Wanafunzi
wengine wa Shule za Fedha ambao ni Prince Mwemezi Muzamil Katunzi,
Goodluck Komba, Sajjad El-Amin na Veronica Samuel Ndomba ambao kila
mmoja ameshinda medali za fedha katika makundi ya ushindani tofauti
chini ya usimamizi wa mwalimu Metin Er wa Masomo ya Biashara, Fedha
International School walieleza kunufaika na mashindano kitaaluma na
upeo.
Mwanafunzi
Mwemezi Muzamil Katunzi, ambaye aliwasilisha picha yenye ujumbe wa
mazingira na kushinda alisema picha hiyo aliipiga eneo la viwanja vya
Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam ikielezea namna binadamu
wanaathiri mazingira kwa kuchoma moto hovyo na kuleta matatizo mengine
duniani. Kwa upande wao wanafunzi Goodluck Komba na Sajjad El-Amin
waliwasilisha andiko la mradi wa kutengeneza mkaa kwa kutumia makaratasi
taka ambao ulishika nafasi ya tatu katika mashindano ya Genius Olympiad
yaliyofanyika jijini New York.
Mwanafunzi
Komba alisema mradi wao ni rafiki wa mazingira na ukitumika utaokoa
sehemu kubwa ya uharibifu wa mazingira. Kwa upande wake msichana pekee
aliyeshinda katika mashindano hayo, Veronica Samuel Ndomba alisema
andiko lake lilishinda kwenye kipengele cha 'Mazingira Yetu' na
aliandika kuonesha namna elimu ya mazingira inaweza kutolewa na kulinda
uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanywa katika shughuli mbalimbali za
binadamu.
Naye
msimamizi wa wanafunzi hao, mwalimu Metin Er alisema kundi hilo la
wanafunzi mbali na kujijenga kimaarifa kwa wanafunzi hao wameiletea sifa
Tanzania kwani kwani mashindano hayo ya kitaaluma yalishirikisha nchi
mbalimbali zikiwemo USA, Romania, Nigeria, Tunisia, Holland,
Turkmenistan, Kazakhstan and Russia. Shule za Fedha International School
zimekuwa zikifanya vizuri kitaaluma kitaifa na kimataifa jambo
linaloendeleza umaarufu wa shule hizo kila uchao. *Imeandaliwa na
www.thehabari.com
No comments:
Post a Comment