Header Ads

Siri 5 za kuwa msanii bora na mwenye mafanikio

 

Siku zote mafanikio huwa hayana  kanuni kamili ya kusema kwamba ukiifwatisha  itakutoa bali huwa kuna vitu ambavyo ukivizingatia unaweza fikia mahali pazuri ambako ni nafuu kuliko ulivyozania. Wasanii wengi katika tansia mbali mbali imewachukua mda kutambua nyenzo gani au njia zipi za kupitia ili waweze fikia malengo na jinsi ya kumudu pindi pale wanapofikia hayo malengo. Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo yapaswa kuzingatia ili uweze fikia mafanikio;
 
 
1. Sanaa iwe kiini cha maisha yako

Unapoamka au kabla haujalala inabidi uwe unafikiria kuhusu sanaa, kitu gani kingine ufanye cha sanaa ambacho kikifikia hadhira kiweze kukongoa nyoyo za mashabiki. Muda wako mwingi utumie kufanya sanaa na jinsi ya kuitangazisha ili iweze fikia wengi maana kazi inaweza ikawa nzuri sema hamna njia ya kufikisha kwa walengwa. Kwa maana nyingine sanaa inabidi iwe kazi yako kwa muda wote , ifanye kwa kujiamini na kwa kupenda bila kushurutishwa.

2. Elewa jinsi sanaa inavyokwenda mkabala na biashara

Msanii inabidi aelewe sekta za ujasiriamali katika sanaa ili aweze ingiza kipato kupitia sanaa hiyo. Kunapokuja njia mpya ya kibiashara katika sanaa, msanii hana budi bali kuelewa njia hiyo, ajue atafaidika vipi na haki zake zipi ili ajiunge nayo moja kwa moja au anaweza akayagawa madaraka hayo kwa msimazi au wasimazi wake ili yeye aweze kuendelea na mambo mengine huku wasimazi waweze msaidia kwenye swala hilo. Hii itaokoa muda na hata kumfanya afike mbali zaidi kama akizingatia.

3. Fanya kazi kwa bidii

Unaweza ukawa ni msanii mzuri na unaipenda kazi yako sema ni mvivu katika utekelezaji wa kazi yako. Hii inaweza kukurudisha nyuma kimaendeleo. Msanii unatakiwa uwe unaipenda kazi yako lakini pia uwe na juhudi ya kufanya kazi yako kwa kuwa mafanikio hayaji hivi hivi. Pindi unatakavyojituma pia itawapa mshawasha hata waliopembeni yako kujitoa zaidi kwa kukusaidia kwa kuwa wanaona unamwelekeo. Ukiwa mvivu utabaki pewa sifa tu lakini hausogei kwa namna moja ama nyimgine kimaisha.


4. Kutokata tamaa

Katika sanaa huwa kuna vitu mbali mbali ambavyo lazima msanii akabiliane navyo ili kufikia malengo. Na vitu hivyo huwa vinakulazimu kufanya kazi ya ziada au kufanya kazi kwa bidii maana kuna kupanda na kushuka katika sanaa sasa pindi pale unapokwama haikupasi kukata tama na kughairi kabisa bali inapaswa uichukulie kama changamoto na kisha ifanyie kazi. Huwezi jua, pale unapokatia tamaa kama ungekomaa na kuendelea kidogo mafanikio kumbe yalikua karibu.


5. Kaa na watu wenye mawazo chanya

Usipende kuzungukwa na watu wenye mawazo hasi na wewe sanasana tukija kwenye upande wa sanaa unayoifanya . Utakuta badala watu wakusaidie kimawazo na ushauri, wao cha kwanza ni kukuambia acha sanaa hiyo kwa sababu zisizo na msingi. Jitahidi kukaa na watu wenye mawazo chanya kiasi kwamba anakupa ushari pindi anapoona umeteleza ama jinsi ya kufikia malengo. Wasanii wengi wakongwe wanaweza kuwa msaada kwako wewe msanii chipukizi kwa kuwa wanaufahamu mkubwa na ujuzi ambao unaweza kukusaidia wewe kwa namana moja ama nyingine. Jifunze toka kwao kisha chukua ya kwao changanya na yako na utajikuta unafika mbali bila kutarajia.

13 comments:

KICHANGANI AREA said...

Ahsanteni

Freld De Mgazwa said...

Asante Nimejifunza Pakubwa

Unknown said...

Maneno kuntu nimejifunza kitu

Anonymous said...

nimejifunza

Anonymous said...

Anonymous said...

Nimejigunza

Anonymous said...

Nimepata kitu ndugu asante sana ntayafanyia kazi, I'm the one to be!✌

Anonymous said...

Nimejifunza ntayafanyia kazi kesho ning,'are kama diamond kwenye tasnia ya music i like it

Anonymous said...

Ok nimepata kitu

Anonymous said...

Good

Anonymous said...

Ala


Claud

Anonymous said...

Mimi claud balaka natangaza kumwimbajimkubwachuya

Anonymous said...

Pamoja sana,🫂🫂

Powered by Blogger.