Header Ads

BOT YAWATAHADHARISHA WANANCHI

 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akimpatia vipeperushi Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, wakati alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya Wiki ya Utumishi, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akimpatia vipeperushi Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, wakati alipotembelea banda la wizara katika maonesho ya Wiki ya Utumishi, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu kazi ya Benki Kuu, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. 
 Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu sarafu ya sh. 500, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. 
Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu sarafu ya sh. 500, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. (Picha zote na Kassim Mbarouk)


Na Salma Ngwilizi – Maelezo
BENKI  ya Tanzania(BOT) imewataadharisha wananchi kwamba  sarafu  ya sh. 500 haina  madini ya aina yoyote na wala haiuzwi haiuzwi  kama inavyoadaiwa na baadhi ya watu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Meneja  Uhusiano wa benki hiyo,  Zalia Mbeo wakati akitoa ufafanuzi kwa  Kaimu  Katibu Mkuu wa  Ofisi ya Rais Menejimenti ya  Utumishi wa Umma, HAB  Mwizu  ambaye aliuliza kwamba  kuna taarifa kuhusu sarafu  hiyo kuuzwa mitaani.

Kaimu Katibu Mkuu huyo ambaye alifungua maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,  Mhe. Celina Kombani.

 “Watanzania wanatapeliwa sarafu hii haina thamani yoyote ni uzushi,” alisema Zalia.
 Aliongeza wananchi wadanganywa na watu kuwa sarafu hiyo ikiyeyushwa ina madini ambayo  yanaweza kuwapatia fedha nyingi  wakati si kweli.
Maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yamefunguliwa rasmi jana Juni 16, mwaka huu na yanatarajia kumalizika Juni 23, mwaka huu.

 Kauli mbiu ya mwaka huu “Utumishi wa Umma katika Bara la Afrika ni chachu ya kuwawezesha Wanawake kuongeza Ubunifu  na Kuboresha utoaji wa Huduma kwa Umma”.

No comments:

Powered by Blogger.