Header Ads

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NDANI YA WILAYA YA BUKOMBE MKOAN GEITA.

Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukivuka mto kuelekea katika kijiji cha Ilyanchele wilayani Bukombe wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika wilaya hiyo kuelekea katika kijiji hicho hata hivyo msafara huo haukuweza kuvuka mto mkubwa wa Ilyamchele na magari  kutokana na kutokuwepo kwa daraja linalounganisha kijiji hicho ambapo leo ndiyo limewekwa  jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo  na Ndugu Abdulrahman Kinana.
Baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa daraja hilo Kinana pamoja na msafara wake walivuka mto huo kwenye daraja la miti lililotengenezwa kwa nguvu za wananchi.  kisha alipanda pikipiki na kuelekea katika mkutano mdogo na wananchi wa kijiji cha Ilyanchele ambacho kimo katika msitu wa akiba  kata ya Nyamonge wilayani Bukombe mkoani Geita.

Kinana yuko katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Kagera, Geita na Mwanza ambapo baada ya kumaliza ziara yake mkoani Kagera sasa anaendelea na ziara hiyo katika mkoa wa Geita kabla ya kumalizia ziara yake mkoani Mwanza akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akivuka na wananchi katika daraja hilo.
Wananchi wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana alipokuwa akiwahutubia mjini Bukombe,mkoani Geita
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwahutubi Wananchi katika mkutano wa hadhara mjini, Bukombe wakati wa ziara yake mkoani Geita.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akitema chehe katika mkutano wa hadhara mjini, Bukombe wakati wa ziara yake mkoani Geita.
Katibu wa NEC Itikadi  na Uenezi Nape Nnauye akiunguruma katika mkutano wa hadhara mjini Bukombe



Wananchi wakimlaki Katibu Mkuu Kinana kwenye mkutano wa hadhara mjini Bukombe,
Wananchi wakimlaki Katibu Mkuu Kinana alipokuwa akiwasili kwenye mkutano wa hadhara mjini Bukombe.
 Katibu Mkuu Ndugu Kinana akishiriki kufitisha fremu ya mlango katika vyumba vya madara ya Shule ya Sekondari ya Busonge, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akishiriki kutega mzinga wa nyuki katika Kata ya Iyogelo, wilayani Bukombem Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana  akiwahutubia wachimbaji wadogo wadogo wa madini katika Kata ya Uyovu, wilayani Bukombe, Geita.
Baadhi ya wachimbaji wadogo wadogo wakitafuta dhahabu wilayani Bukombe.
 Ndugu Kinana akizungumza na wajasiliamali wa uuzaji wa samaki na dagaa katika Soko la Uyovu katika Kata ya Uyovu, wilayani Bukombe.
Wananchi wa Kijiji cha Ilyamchele wakisindikiza kwa ngoma msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana na Nape Nnauye
 Komredi Kinana akishiriki ujenzi wa chumba cha darasa katika Shule ya Msingi ya Ilamchele, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita.
Sehemu ya chumba cha darasa cha Shulre ya Msingi Ilyamchele, katika Kata ya Namonge, wilayani Bukombe. Ndugu  Kinana baada ya kuona hali hiyo, aliitisha harambee ya ujenzi wa shule hiyo, isiyokuwa na walimu wataalamu
 Ujenzi wa vyumba viwili vya darasa katika Shule ya Msingi ya Ilyamchele ukiendelea, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitumia usafiri wa pikipiki alipokuwa anakwenda Kijiji cha Ilyamchele, Kata ya Namonge ambako aliendesha harambee ya ujenzi wa Shule ya Msingi ya Ilyamchele akiwa katika ziara wilayani Bukombe, Geita, ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi cya chama hicho pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Wananchi wakivuka daraja la Ilyamchele wilayani Bukombe, Geita

Wananchi wakivuka daraja la Ilyamchele wilayani Bukombe, Geita
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akivunja muwa na baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Bukombe wakati akirejea mara baada ya mkutano wake na wananchi wa kijiji cha Ilyanchele.
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akichagua muwa na baadhi ya watendaji wa Halmashauri ya Bukombe wakati akirejea mara baada ya mkutano wake na wananchi wa kijiji cha Ilyanchele.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akizindua ujenzi wa wa dara la Ulyamchele,wilayani Bukombe mkoani Geita.
 Gari lililombeba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye likivuka katika moja ya mito katika Kijiji cha Ilyamchele, wilayani Bukombe.
 Msafara wa Komredi Kinana ukivuka katika moja ya mio iliyopo Barabara ya Ilyamchele
Komredi Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la CCM  Tawi la Busonzo, wilayani Bukombe

No comments:

Powered by Blogger.