Header Ads

TAMWA Kuwajengea Uwezo Waandishi Uandishi Habari za Uchaguzi

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Gradness Munuo akizungumza na baadhi ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na wahariri hao. 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Gradness Munuo akizungumza na baadhi ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na wahariri hao.Sehemu ya wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) na kufanyika leo jijini Dar es Salaam.Sehemu ya wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa katika mkutano ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) na kufanyika leo jijini Dar es Salaam.

CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kimepanga kuwajengea uwezo baadhi ya waandishi wa habari nchini juu ya uandishi wa habari za uchaguzi kujiandaa na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 2015. 

Akizungumza katika mkutano na baadhi ya Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Gradness Munuo alisema mafunzo hayo yatawaongezea ujuzi wanahabari juu ya uandishi wa habari za uchaguzi kwa ujumla kwa kuzingatia utoaji wa nafasi kwa makundi ya wanawake, 

vijana na watu wenye ulemavu. Alisema kundi la wanawake wanaoshiriki kugombea katika nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi na walemavu wamekuwa wakikosa fursa kwenye vyombo vya habari kujinadi kutokana na mfumo na mazingira ya uchaguzi yalivyo, hivyo kuna haja ya kuwajengea uwezo wanahabari ili waweze kuzipa kipaumbele pia na makundi hayo ambayo huachwa nyuma kwenye mchakato mzima.

No comments:

Powered by Blogger.