TAMASHA LA QASWIDA SASA KUFANYIKA MEI 31 JIJINI DAR

Pichani kati ni Mkurugenzi
wa Taasisi ya Ulamaa Qaswida Promotion Centre,Jumanne
Ali Ligopora akizungumza na waandishi wa
habari kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar es salaam
kuhusiana na tamasha la Qaswida,linalotarajiwa kufanyika kwenye viwanja
vya shule
ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa
mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe.Kulia ni Sheikh Muharami
Pembe
na kushoto ni Ustaadhi Jumanne Gereza. 

Mmoja
wa watakaoshiriki katika tamasha hilo,Rahma Muhidin Kigora akighani
Qaswida mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani).

Baadhi ya Waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo uliohusu
tamasha la Qaswida,linalotarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe.Kulia ni Sheikh Muharami Pembe na kushoto ni Ustaadhi Jumanne Gereza.
tamasha la Qaswida,linalotarajiwa kufanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe.Kulia ni Sheikh Muharami Pembe na kushoto ni Ustaadhi Jumanne Gereza.
Tamasha la Qaswida lililokuwa
likitarajiwa kufanyika Mei 25,jijini Dar,sasa limepangwa kufanyika Mei 31
katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,ambapo mgeni rasmi anatarajiwa
kuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe.
Akizungumza na Waandishi wa
habari mapema leo,kwenye hoteli ya Traveltine Magomeni jijini Dar, Mkurugenzi
wa Taasisi ya Ulamaa Qaswida Promotion Centre,Jumanne Ali Ligopora amesema kuwa
tamasha hilo limebadili tarehe ya onesho lake ili kuwa bora zaidi.
Amesema kuwa tamasha hilo
ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake,tayari lmekwishawapata wadhamini
watatu,amewataja wadhamini hao kuwa ni Gazeti la Dira ya Mtanzania, watengenezaji
wa kinywaji cha Sayona na Madrasamtimun.
Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa katika
mashindano hayo kutakuwepo na watu wa benki za miamala ya kiislam,ambao
wataonesha namna benki hizo zinavyofanya kazi na huduma kwa wateja wao.
No comments:
Post a Comment