Header Ads

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NDANI YA JIMBO LA VUNJO MKOANI KILIMANJARO

   Wananchi wa Kata ya Makuyuni wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye aliwaambia kwa miaka mingi sasa jimbo la Vunjo limekuwa linarudishwa nyuma na ushabiki wa kisiasa na kuwataka wananchi hao kufanya maamuzi sahihi mwaka huu kwa kuichagua CCM.
 katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisikiliza moja ya swali lililokuwa likiulizwa na mmoja wakazi wa himo,Bi.Pepetua Shayo kuhusiana na mradi wa maji uliopo katika eneo hilo,ambapo baadhi ya wananchi wamechukuliwa maeneo yao bila kulipwa fidia yoyote.

 Kijana kutoka chama cha Chadema Membeck Kaigarula akikabidhi kadi ya Chadema kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na kutangaza rasmi kujiunga na CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Himo. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi kwenye uwanja wa polisi Himo ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa muda umefika sasa wa kufanya maamuzi ya msingi kwa kuchagua kiongozi anayeweza kuleta maendeleo katika Jimbo la Vunjo.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia kwenye mkutano wa hadhara uliofanyiaka kwenye viwanja vya polisi himo na kuwaambia wananchi hao wapinzani hawana tena ubavu wa kuongoza kwani kwa zaidi ya miaka mingi sasa wamepata nafasi na hamna walichokifanya kwa wananchi hao wa jimbo la Vunjo.
 Naibu Kamanda wa UVCCM  Moshi Vijijini,Innocent Shirima akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Moshi mjini,Mh.Novatus Makunga,kabala ya kuelekea kwenye mkutano wa hadhara ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alihutubia wakazi wa Vunjo. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnaupe pichani kushoto na wajumbe wangine wakitembea kuelekea kwenye uwaja wa mkutano wa hadhara,mjini himo.
 Katibu Mkuu wa CCM akinunua ndizi barabarani Himo wakati akielekea kwenye uwanja wa mkutano wa hadhara
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kufyatua matofali kwenye mradi wa vijana wa kijiji cha Oria ,kata ya Kahe Magharibi. 
Baadhi ya wananchi wakishangilia jambo kwenye uwanja wa polisi Himo ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa muda umefika sasa wa kufanya maamuzi ya msingi kwa kuchagua kiongozi anayeweza kuleta maendeleo katika Jimbo la Vunjo.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na Naibu Kamanda wa UVCCM  Moshi Vijijini,Innocent Shirima alipokuwa akiwasili katika kijiji cha Oria,Kata ya Kahe Magharibi,jimbo la Vunjo

No comments:

Powered by Blogger.