ASILIMIA 40 YA WANAWAKE Z’BAR WANAISHI MAISHA DUNI

Mke
wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi
(aliyefunikwa mwamvuli) akiwasili kwenye sherehe ya siku ya wanawake
duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika ndani
ya ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel mwishoni mwa wiki.
Na Mwandishi wetu, Zanzibar
UTAFITI
uliofanywa na taasisi ya wanawake nchini Zanzibar ya Zanzibalicious
Women umeonyesha kuwa asilimia 40 ya wanawake Zanzibar, wanaishi katika
mazingira duni ya umasikini kwa kutojitambua na kukosa elimu ya uelewa
jinsi ya kukabiliana na mazingira waliyomo.
Akisoma
risala siku ya wanawake mbele ya mgeni rasmi mke wa rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mama Mwanamwema Shein , katika
siku ya wanawake hafla iliyofanyika hoteli ya Bwawani, Mweka hazina wa
Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal alisema hali hiyo ni changamoto
kubwa na sasa kunatafutwa namna ya kumfikia mwanamke huyu ambaye
ameshagota katika jamii yetu.
“Mama
Shein asilimia hii ni kubwa saana, na sisi kama wanawake ambao tayari
tumejaaliwa elimu na tunajitambua, ikiwa ni pamoja na tayari tumepiga
hatua kimaendeleo katika nyanja mbalimbali, tumeguswa sana sana na
suala hili.” Alisema Shekha.
Zanzibalicious
ni umoja wa wanawake wanaoishi Zanzibar,ulioanzishwa mwaka 2011,na
kusajiliwa rasmi mwaka 2013, ikiambatana na uzinduzi uliofanyika tarehe
28 Machi 2014.

Mke
wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama
Mwanamwema Shein akiwasili kwenye sherehe ya siku ya Wanawake duniani
iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group mwishoni mwa wiki katika
ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel.
No comments:
Post a Comment