Kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni
Picha juu na chini ni mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la Bingwa, Dimba na
Mtanzania kutoka Kampuni ya New Habari 2006 Ltd, Sharifa Mmasi pichani
akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni kilichoandikwa na Kambi
Mbwana, ambaye ni Mratibu Mkuu wa Tamasha la Handeni Kwetu
linalofanyika kila mwisho wa mwaka wilayani Handeni, mkoani Tanga.
MWANDISHI wa Habari za Michezo ambaye pia ni Mratibu Mkuu wa
Tamasha la Utamaduni la Handeni Kwetu, Kambi Mbwana, ameandika kitabu chake kinachojulikana
kama ‘Dira na Tumaini Jipya Handeni’, kilichoanza kupatikana mapema wiki hii jijini
Dar es Salaam na wilayani Handeni, mkoani Tanga.
Sharifa Mmasi akisoma kitabu cha Dira na Tumaini Jipya Handeni, kilichoandikwa na Kambi Mbwana.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mbwana alisema kwamba
kuandika kitabu hicho kuna lengo kubwa la kuelimisha jamii kwa ajili ya
kutafuta fursa ya kimaendeleo katika wakati huu ambao wananchi wengi wamekuwa
wakilia bila kupata msaada wowote.
“Naijua vizuri wilaya yangu ya Handeni na mkoa wa Tanga kwa
ujumla, hivyo nimeamua nitumie kipaji change katika kuandika kitabu hiki
ambacho kimeweza kuanika mambo mengi yenye tija kwa serikali na wananchi kwa
ujumla, hivyo naomba waniunge mkono kwa kuhakikisha kwamba wanapata kitabu hiki
popote kitakapokuwapo.
No comments:
Post a Comment