Header Ads

Wananchi wa Vunjo wamchangia Innocent Melleck shirima kuchukua fomu ya ubunge vunjo

 WANANCHI  wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro wakiwamo wajasiliamali wadogo wamechangishana shilingi milioni tisa na kumkabidhi Naibu  Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Innocent  Melleck  kwa ajili ya kuchukulia fomu ya kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Wakizungumza na waandishi wa habari kwenye mji mdogo wa himo baadhi ya wananchi hao Halid Msango,Jonas Mamuya na Aisha Mkwizu walisema kwa pamoja wananchi wa jimbo la Vunjo bila kujali itikadi zao za vyama wamemchangia kiasi hicho cha fedha ili kimsaidie kuchukulia fomu ya kugombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), muda utakapofika.
unnamed Katika tukio hili tumeshiriki wananchi wa jimbo hili la Vunjo kwa umoja wetu bila kujali itikadi za kisiasa ambapo hapa pia wapo wanachama wa vyama vya NCCR Mageuzi,TLP,CHADEMA na CCM  soote tumeshiriki katika kuchanga fedha hizi lakini pia wapo makundi mbalimbali kama vile mama lishe, madereva wa Bodaboda, wauza mboga, na vijana wengine wanaofanya biashara ndogondogo na wapiga debe kwenye vituo vya mabasi ya daladala.

Aidsha wananchi wao waliafikiana kuunda kamati ya kuzunguka jimbo zima kuhakikisha kuwa wanakusanya fedha za michango na kuhamasishana kwaajili ya kuhakikisha Melleck anapata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Katika kamati hiyo mwenyekiti ni Mzee shayo na katibu wa mwika kuwa katibu huku katibu kata kata ya kilema kusini Shabani Kwezi kuwa mjumbe na wajumbe wawili toka kila kata za jimbo hilo hivyo kuwa na jumla ya wajumbe 36 katika kamati hiyo ambayo ilianza majukumu yake mara moja.

Alisema zoezi hilo liliongozwa na zaidi ya wajumbe 1000 wa nyumba 10 wa CCM na kumtaka, Melleck kuchukua fomu ya kuwani nafasi hiyo ya uwakilishi katika uchaguzi ujao.
  Kwa upande wake Bwana Melleck aliwashukuru wananchi hao kwa ujasiri mkubwa na Imani kubwa walioonyesha kwake , nimefarijika sana kuona wananchi wenye kipato kidogo cha fedha wanachanga kiasi hiki cha fedha na kunikabidhi ili nichukulie fomu na mimi naahidi kutowaangusha kwa hilo, nitafanya hivyo muda ukifika,” alisema .

No comments:

Powered by Blogger.