Header Ads

WAFANYAKAZI HOTELI YA SNOWCREST ARUSHA WALILIA MISHAHARA YAO

Moses Mashalla,Arusha

Baadhi ya watumishi katika hoteli yenye hadhi ya nyota nne ya Snowcrest Hotel ya jijini Arusha wameushutumu uongozi wa hoteli hiyo kwa kushindwa kuwalipa mishahara yao tangu mwezi Januari hadi sasa.

Pia wameiangukia serikali  kwa kuitaka iingilie kati suala hilo kwa kuwa pamoja na kuwasilisha madai yao katika idara mbalimbali za serikali mkoani hapa lakini hadi sasa wameshindwa kupatiwa ufumbuzi wa madai yao.

Hoteli hiyo ni ile ambayo ilizinduliwa na Rais Jakaya Kikwete  mwaka 2009 na kisha kuvunjwa ghafla na Wakala wa barabara mkoani Arusha(Tanroads) baada ya ukuta wake kudaiwa kujengwa katika eneo la hifadhi  ya barabara ya Arusha-Moshi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti watumishi hao kwa sharti la kutotajwa majina yao hadharani kwa sababu za kiusalama walidai kuwa uongozi wa hoteli hiyo umeshindwa kuwalipa mishahara yao tangu mwezi Januari hadi sasa.

Wakiongea kwa nyakati tofauti na gazeti hili walidai kuwa kitendo cha wao kutolipwa mishahara yao kimechangia ukali wa maisha kwa kuwa baadhi yao wameshindwa kuwapeleka watoto wao mashuleni na hata kushindwa kumudu kulipia kodi za nyumba zao.

No comments:

Powered by Blogger.