Header Ads

CHUO CHA TAKWIMU MASHARIKI MWA AFRIKA KUTILIANA SAINI YA MKATABA WA MAKUBALIANO YA MAFUNZO YA WATALAAM WA TAKWIMU NA CHUO CHA TAKWIMU CHA INDIA.

Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) kimekamilisha maadalizi ya kutiliana saini ya mkataba wa makubaliano ya mafunzo ya Watalaam wa Takwimu na Chuo cha Takwimu cha nchini India.
 
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo cha EASTC Prof. Innocent Ngalinda amesema mkataba huo utasainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
 
“Maandalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu na Chuo cha Takwimu cha nchini India yamekamilika kwa kiasi kikubwa na ndio maana hapa mbele yenu mnamuona Naibu Balozi wa Ubalozi wa India hapa nchini amefika kwa ajili ya kujirizisha”, amesema Prof. Ngalinda.
 
Prof. Ngalinda amesema kuwa mkataba huo una manufaa makubwa kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa wataalam wengi katika tasnia ya takwimu hapa nchini.
 
Pamoja na ongezeko la watalaam wa takwimu hasa wakufunzi, kutakuwa na ukarabati wa miundombinu katika chuo hicho ambapo mabweni ya wanafunzi pamoja na ofisi za chuo hicho zitakarabatiwa.

No comments:

Powered by Blogger.