Header Ads

KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AMNUSURU MBUNGE WA IGALULA MFUTAKAMBA BAADA YA WANANCHI WAKE KUMJIA JUU


Wakazi wa Kata ya Kizengi wakishangilia jambo,wakati Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akizungumza nao,mara baada ya kuweka jiwe la msingi na  kuzindua Ofisi ya chama hicho.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Kata ya Kizengi,Wilayani Uyui mkoani Tabora,wakati wa ziara yake iliyoendelea mkoani humo.Kinana amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi ili kuchukua hatua na kuzishughulikia,aidha katika ziara hiyo Kinana pia ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye.

Ndugu Kinana amehutubia mamia ya wananchi kwenye mkutano hadhara uliofanyika katika Kata ya Loya,ambapo kuliibuka sintofahamu ya baadhi ya mambo ikiwemo Mbunge wa Jimbo Igalula, Mhandisi  Athuman Mfutakamba kutokuwa na tabia ya kuwatembelea wananchi wake na kujua matatizo waliyonayo, hali iliyosababisha Wananchi wamzomee alipopanda jukwaani kuhutubia na kujibu maswali aliyoulizwa  ambapo ilibidi Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kuingilia kati na kurejesha hali ya utulivu na kumtaka Mbunge wa jimbo hilo Mh,Athumani Mfutakamba kuwa na tabia ya kuwatembelea wananchi wake.

Aidha kauli hiyo imekuja,kufuatia Wananchi kulalamika wazi kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na kutokubali utendaji kazi wa Mbunge huyo.Wananchi hao waliweka wazi kuwa Mbunge huyo amekuwa akipiga porojo tu kwa mambo mengi ,badala ya kuwasikiliza na kutatua matatizo yanayowakabili amekuwa akiingia mitini.

Wananchi hao wakatolea mfano wa  Zahanati ya Kata hiyo ambayo haina jokofu la kuhifadhia chanjo za watoto na Dawa,kwamba aliahidi kulishughulikia lakini hakuna utekelezaji uliofanyika hadi sasa,kama vile haitoshi Wananchi hao wakoangeza kuwa mara baada ya kuchaguliwa Mbunge huyo aliwaahidi kuwaletea mnara wa mawasiliano ya simu za mikononi kwa muda wa siku 100,ambalo ndio tatizo kubwa kwa kata hiyo ya Loya,lakini hakulitekeleza mpaka sasa.

Hata hivyo katika kuweka mambo sawa kwa Mbunge huyo,katibu Mkuu wa CCM,Ndugu kinana aliwaeleza wananchi kuwa atawasaidia kufuatilia suala hilo la mawasiliano,na pia amewaahidi kuwanunulia jokofu hilo kwa wananchi wa Kata ya Loya wilayani Uyui mkoani Tabora.
Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye,akiwahutubia wakazi wa Kata ya Kizengi waliojitokeza kwa wingi,Wilayani Uyui mkoani Tabora,kwenye mkutano wa hadhara.
Mbunge wa Jimbo la Igalula,Mh.Athuman Mfutakamba,akieleza maendeleo ya miradi mbalimbali iliyotekelezwa na chama cha CCM,kufuata Ilani ya chama hicho,katika Lijiji cha Loya,Wilayani Uyui mkoni Tabora.
Mwenyekiti wa CCM,Wilaya ya Uyui,Mussa Ntimizi akizungumza na Wananchi wa Kata ya Kizengi wakati akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi katika Ofisi ya chama hicho na kuzungumza na wananchi.
Wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara uliofanywa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana katika kijiji cha Loya,Wilaya ya Uyui.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (hayupo pichani) akisomewa taarifa fupi mara baada ya kukagua ujenzi wa nyumba mbili za waalimu wa Shule ya Sekondari Lutende,Wilayani Uyui mkoani Tabora.
Ndugu Kinana akizungumza na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Miyenze,ambapo paalibulika na hoja ya mgogolo mkubwa wa wafugaji na Wahifadhi uliodumu kwa muda mrefu.




Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiweka jiwe la msingi kenyew Ofisi ya CCM,kata ya Loya wilayani Uyui mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa CCM,Wilaya ya Uyui,Mussa Ntimizi na Mbunge wa Jimbo la Igalula,Athumani Mfutakamba, wakisalimiana na  baadhi ya vijana wa michezo mara walipowasili katika kata ya Loya,kwa ajili ya mkutano wa hadhara na wananchi.




Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Loya,katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo,Wilayani Uyui mkoni Tabora.
Katibu wa NEC,Itikadi Siasa na Uenezi,Ndugu Nape Nnauye akihutubia Wananchi,katika kijiji cha Loya,Wilayani Uyui mkoni Tabora.
Vijana wa Sungusungu wakicheza wakati wa kumpokea Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akiwasili katika kata ya Kizengi,wilayani Uyui kuweka na kuzindua Ofisi ya chama hicho na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Vijana wa Sungusungu na Baadhi ya Wazee wa Kata ya Kizengi wakimpokea Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe wake walipokuwa wakiwasili katika kata ya Kizengi,wilayani Uyui kuweka na kuzindua Ofisi ya chama hicho na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.

No comments:

Powered by Blogger.