Header Ads

Muungano wa Tanzania ni kielelezo cha maendeleo.



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais( Muungano) Samia Suluhu Hassan akiongea na waandishi wa habari( Hawapo Pichani) kuhusu mafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika utekelezaji wa masuala ya Muungano wakati wa Mkutano leo Mjini Dodoma. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Habari wa Ofisi hiyo Bi. Siglinda Chipungaupi.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais( Muungano) Samia Suluhu Hassan leo mjini Dodoma.

(PICHA NA HASSAN SILAYO)


Na Jovina Bujulu
Muungano wa Tanzania umeendelea kuwa nyenzo na utambulisho muhimu katika kuleta umoja na maendeleo katika taifa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mh. Samia Suluhu Hassan wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo mjini Dodoma.

“Miaka 50 ya Muungano imekuwa ni ya mafanikio makubwa ambayo yamewanufaisha wananchi katika nyaja mbalimbali kijamii, kiuchumi, na Kisiasa” alisema Waziri Suluhu.

Waziri Samia alisema kuwa muungano huo umeendelea kuwa kielelezo imara katika suala la ulinzi na usalama hali iliyowezesha kuwepo kwa amani na utulivu nchini.

Katika suala la haki za binadamu Waziri Samia alisema kuwa suala hilo limeendelea kupewa kipaumbele ndani ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo wananchi wameendelea kupata haki zao za msingi kupitia mahakama za Mwanzo hadi za Juu.

Akifafanua kuhusu suala la elimu Waziri Samia alibainisha kuwa wanafunzi wenye sifa Tanzania Bara na Zanzibar wanapatiwa mikopo ili kukidhi gharama za Masomo, hali iliyosabisha uimarishwaji wa elimu ya juu kwani kuwekuwepo kwa ongezeko la vyuo vya elimu ya juu kutoka 25 mwaka 2015 hadi 63 vilivyopo sasa.

Aidha Waziri Samia alisema kuwa Serikali hizi mbili zinashirikiana katika kubuni na kuibua miradi ya Maendeleo inayofadhiliwa na Serikali kwa Kushirikiana na Wahisanai wa Maendeleo.

“Serikali hizi zimekuwa na ushirikiano wa pamoja katika masuala ya mandeleo mfano Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF III, MACEMP, ASDPL na ASDP kwa ujumla imekuwa ni chachu kubwa ya Maendeleo ya wananchi katika pande zote za Muungano” Alisema Waziri Samia.

Waziri Samia aliongeza kuwa Maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano yalizinduliwa Zanzibar tarehe 1 Machi na Rais wa Zanzibar Dkt. Ally Mohamed Shein ambapo nembo ya Muungano ilizinduliwa na sherehe za Muungano zitafanyika Dar es Salaam.


Kauli mbiu ya Mwaka huu ni “Utanzania wetu ni Muungano wetu, Tuulinde, Tuumarishe na Kuudumisha.”

Doreen Noni kushiriki shindano la Africa Magic Choice Awards Lagos

DSC_0041
Mjasiriamali na Mbunifu wa mavazi nchini Tanzania, Doreen Noni akizungumza kwenye Exclusive Interview na mtandao wa habari wa MOblog.

Na Damas Makangale, MOblog Tanzania

MJASIRIAMALI na Mbunifu wa mavazi nchini Tanzania, Doreen Noni anatarajiwa kushiriki kwenye shindano la kumtafuta mbunifu bora katika sanaa ya filamu, (Africa Magic Viewers Choice Awards) nchini Nigeria wiki hii.

Akizungumza na MOblog Tanzania, hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Noni amesema kwamba amechaguliwa kushiriki katika shindano hilo la Africa Magic Viewers Choice Awards baada ya kushiriki filamu ya siri ya mtungi. “Africa magic viewer’s choice awards ni kama Oscar ya Afrika ambapo sinema zote wanazotizama watu kwenye Mnet, series na nia hasa ni kutizama kazi za wasanii mbali katika fani ya uingizaji wa filamu Afrika,” amesema.

Amesema alifanikiwa kufanya kazi na kampuni ya (Media for Development International) ambao wanafanya kazi ya kuhamasisha kazi za uzalishaji katika filamu za Afrika ili kutambua mchango wa wasanii mbalimbali katika bara hili.
DSC_0128
Noni amesema kuwa kupitia kampuni au shirika hilo lisilo kuwa la kiserikali aliweza kushiriki kwenye filamu ya “Siri ya Mtungi” ambapo alitengeneza nguo na mavazi yote yaliyotumika katika filamu hiyo.

Amesema kwamba katika filamu hiyo alitengeneza nguo kwa kila mshiriki wa filamu baada ya kuzunguka katika masoko mengi ya jijini Dar es Salaam katika kutafuta nguo zinazoendana. “nimechaguliwa baaada ya kupeleka baadhi ya kazi zangu za kisanii hasa kwa design na kubuni mavazi mbalimbali baada ya kuonyesha kipaji chake katika tamthilia hiyo ya Siri ya Mtungi,” alilisitiza.

Noni amesema kwamba yeye ana malengo yake kama kijana na mjasirimali ni kufika mbali katika fani yake hiyo ya ubunifu wa mavazi na ujasiriamali. MJASIRIAMALI na mbunifu wa mavazi anayekuja juu nchini Tanzania, Doreen Noni anatarajiwa kushiriki kwenye shindano la kumtafuta mbunifu bora katika sanaa ya filamu, Africa Magic Choice Awards nchini Nigeria.

No comments:

Powered by Blogger.