 Taarifa zilizolifikia Mwananchi Jumapili na kuthibitishwa na Zitto jana 
jioni zilieleza kuwa Eurodad ambao ni mtandao wa mashirika yasiyo ya 
kiserikali 48 kutoka nchi 19 za Ulaya, yanayojihusisha na masuala ya 
kufuatilia madeni ya nchi zinazoendelea, kwa muda sasa umekuwa 
ukipambana na watu wanaokwepa kulipa kodi. Picha na Maktaba.
Taarifa zilizolifikia Mwananchi Jumapili na kuthibitishwa na Zitto jana 
jioni zilieleza kuwa Eurodad ambao ni mtandao wa mashirika yasiyo ya 
kiserikali 48 kutoka nchi 19 za Ulaya, yanayojihusisha na masuala ya 
kufuatilia madeni ya nchi zinazoendelea, kwa muda sasa umekuwa 
ukipambana na watu wanaokwepa kulipa kodi. Picha na Maktaba.
DAR ES SALAAM.
WAKATI ikisubiriwa ripoti ya uchunguzi wa Tume 
Maalumu iliyoundwa kwa Azimio la Bunge kuchun
guza kashfa ya vigogo 
walioficha Sh323.4 bilioni katika benki nchini Uswisi, Shirika la 
Kimataifa la Mtandao wa Ulaya wa Madeni na Maendeleo (Eurodad), leo 
linaanza kuwachunguza walioficha mabilioni hayo ya fedha nchini humo.
Kazi hiyo ya uchunguzi inaanza leo hadi Novemba 5,
 mwaka huu, ambapo pamoja na mambo mengine watafanya ziara ya uchunguzi 
kuhusu masuala ya uwazi katika kodi katika nchi za Ulaya.
Uchunguzi huo utafanywa na jopo la wataalamu 
waliobobea katika masuala ya kodi na maendeleo na wataongozwa na 
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe ambaye pia
 ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema.
Sakata la kashfa hiyo liliibuliwa bungeni kwa hoja
 binafsi ya Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, mwishoni 
mwa mwaka 2012.
Zitto alisema kwamba kiasi cha fedha kilichofichwa nchini Uswisi ni kikubwa zaidi ya hicho kilichotajwa.
Kufuatia hoja hiyo, Bunge chini ya Spika Anne 
Makinda liliipa Serikali kipindi cha mwaka mmoja ambacho kinaishia 
Oktoba mwaka huu, iwe imekamilisha uchunguzi na kuwasilisha ripoti hiyo 
bungeni.
Ripoti ya Tume hiyo iliyoundwa na Serikali kwa 
Azimio la Bunge ilitolewa mwishoni mwa mwaka jana, ikiongozwa na 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, mpaka sasa 
tayari imewahoji vigogo 200 wakiwamo wabunge, wanasiasa na 
wafanyabiashara.
Muda wa tume hiyo kufanya uchunguzi unakamilika 
mwezi huu na inatarajiwa katika mkutano ujao wa Bunge unaoanza Oktoba 29
 mjini Dodoma, itawasilisha ripoti hiyo.
Taarifa zilizolifikia Mwananchi Jumapili na 
kuthibitishwa na Zitto jana jioni zilieleza kuwa Eurodad ambao ni 
mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali 48 kutoka nchi 19 za Ulaya, 
yanayojihusisha na masuala ya kufuatilia madeni ya nchi zinazoendelea, 
kwa muda sasa umekuwa ukipambana na watu wanaokwepa kulipa kodi.
“Mashirika haya yamekuwa kwenye kampeni ya kupinga
 utoroshwaji wa fedha kupitia ukwepaji kodi unaofanywa na mashirika ya 
kimataifa kwa nchi zinazoendelea,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa kesho Zitto atakutana 
na Waziri wa Fedha wa Uswisi na maofisa wa benki mbalimbali na asasi za 
kiserikali zilizopo katika mji mkuu wa nchi hiyo, Geneva.
“Zitto pia atahudhuria mkutano wa Kamati ya Kodi 
ya Umoja wa Mataifa katika kampeni ya kubadili mfumo wa kodi za 
kimataifa ili kuzuia unyonywaji wa nchi za Kiafrika unaofanywa na 
kampuni kubwa za kimataifa,” inaeleza taarifa hiyo. MWANANCHI
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment