RAIS JAKAYA KIKWETE NA MAMA SALMA WATEMBELEA WILAYA ZA WANGING'OMBE NA MAKETE,MKOANI NJOMBE
Rais 
Jakaya Kikwete akikata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Chuo cha 
VETA cha Wilaya ya Makete  tarehe 19.10.2013 kilichojengwa katika Mji wa
 Iwawa, Makao Makuu ya wilaya hiyo. KatIka hafla hiyo uongozi wa Chuo 
hicho umeamua kukipa jina la Jakaya Kikwete kwa jitihada zake 
alizowezesha wilaya ya Makete kuwa ya kwanza nchini kuwa na chuo cha 
VETA cha wilaya. Kulia kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Elimu NA Ufundi Dr.
 Shukuru Kawambwa na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Makete Ndugu Josephine
 Matiro.
Rais 
Jakaya Kikwete akifuatana na Mkewe Mama Salma wakitembelea Chuo cha VETA
 cha Makete  na kuangalia shughuli mbalimbali zinazofanywa na wanachuo 
wa chuo hicho mara tu baada ya kukizindua rasmi tarehe 19.10.2013. 
Rais 
Jakaya Kikwete na Mama Salma wakipata maelezo ya namna gani ya kupata 
udongo unaofaa kwa ajili ya kufyatua matofali kutoka kwa  Geofrrey Sanga
 na Abel Mbilinyi, wanachuo  wa mwaka  wa kwanza wa chuo hicho.
Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na wananchi mbalimbali waliofika 
kuwapokea wakati walipowasili kwenye kijiji cha Kipengere tarehe 
19.10.2013.
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment