Header Ads

BREAKING NEWS: 

MAKAMU WA MKUU WA CHUO PROF IDRISA KIKULA ATETA NA WANAFUNZI WA UDOM USIKU HUU

Makamu Mkuu Wa Chuo Prof Idrisa Kikula Aongea na wanafunzi mbele ya bweni namba tatu kuwaeleza wanafunzi kuhusu ujumbe aliopewa na serikali.
Katika Hali aliyokuwa akielezea Ujumbe aliotumwa Na serikali kuwa serikali imesema kuwa wanafunzi  wataenda kufanya mafunzo kwa vitendo na pesa zitaingia kabla ya kuanza mitihani ya mwisho ambao inatarajiwa kuanzia jumatatu ijayo.

Wanafunzi hao wameonyesha kukataa ujumbe ulioletwa na Makamu Mkuu Wa Chuo Prof Idrisa Kikula na kuendelea kushikilia misimamo yao kuwa kesho mgomo uendelee kwa sababu walishawahi kuahidiwa na Mawaziri Shamsi Vuai Nahodha na Shukuru Kawambwa na Waziri Mkuu Mh Pinda halafu hakuna kitu na kuchukulia hii ni kama siasa na ndio maana wanafunzi wamegoma na wamekataa kukubali ombi lililoletwa na Makamu Mkuu Wa Chuo Prof Idrisa Kikula.

Wakati huo Huo Waziri Mkuu Wa Serikali ya Wanafunzi Amenusurika Kupigwa Kwa kile kinachosemekana amewasaliti Wenzao. Mpaka Muda huu hali si shwari UDOM na Hali bado haijajulikana 
Tuendelee Kuvuta Subira Kujua Kama Kesho Mgomo Hupo Au Haupo.

Mchezaji wa timu ya Simba Mussa Hassan Mgosi akiwa amembeba mchezaji mwenzake Amri Kiemba mara baada ya kupachika goli la kwanza na la ushindi, katika goli la timu ya Motema Pembe kutoka DRC kwenye mchezo wa michuano ya Kombe la Shirikisho la CAF, uliochezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jioni hii, goli hilo limefungwa kipindi cha kwanza dakika ya 20 ya mchezo huo mshabuliaji Mgosi aliipokea pasi nzuri kutoka kwa kiungo Mohamed Banka kufunga goli hilo pekee, hivyo Simba imefanikiwa kuwatoa "ulimi nje" wapinzani wao Motema Pembe ya DRC.
Mchezaji Emmanuel Okwi akimtoka beki wa timu ya Motema Pembe katika mchezo wa Kombe la Shirikisho la CAF katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mshika kibendera akiangalia wakati wachezaji wa timu ya Simba na Motema Pembe wakichuana katika mchezo wao unaofanyika sasa kwenye uwanja wa Taifa
Mashabiki wa timu ya Simba wakiangalia mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Credits: Full Shangwe Blogu 

 

 

Hii ilikuwa jana pale Chang'ombe TCC Club kwenye show ya GRAND MALT. Wasanii waliotumbuiza ni pamoja na Chege & Temba, Chidi Beenz & Chiku K pamoja na Joh Makini.

Kwa steji ni Joh Makini

 Nikiwa mtamboni kwenye show ya Joh


 Chidi Beenz na LA Familia
Credits: Bongo Star Link

 

 

 

JUST IN:HATIMAYE UNIVERSITY OF DODOMA (UDOM) KESHO KUGOMA MARA BAADA YA KUAMBIWA RASMI KUWA HAKUNA MAFUNZO KWA VITENDO

Wanafunzi wa Kitivo Cha Sayansi ya Jamii, Sanaa na Lugha wakusanyika Mchana huu Kwaajili ya kuamua maswala mazima ya mafunzo kwa vitendo.
Wanafunzi wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokua yakitolewa na Raisi wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii Mh Mwakibinga Philipo Juu Ya Mambo yaliyoweza kufanywa na Serikali mpaka mchana.
Wanafunzi Wa Udom Wakiwa wenye shauku ya kutaka kujua uamuzi utakaochukuliwa na uongozi wa wanafunzi mchana huu katika uwanja wa mpira wa kikapu na mbele ya bweni namba tatu

Wanafunzi Wakitawanyika Mara baada ya Raisi wa kitivo kuwapa uwezo wa kuamua mara baada ya mada iliyotakiwa kuamuliwa na bunge kuwaa tata na kurudishwa kwa wanafunzi ili iweze kuamriwa kama katiba ya serikali ya wanafunzi inavyoeleza
Umati wa wanafunzi ukiwa umekusanyika mbele ya bweni namba tatu na kwenye uwanja wa mpira wa kikapu wakisikiliza maelezo kutoka kwa Raisi wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii mchana huu
 Wanafunzi wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii, Sanaa na Lugha wakiendelea kusikiliza kwa makini uamuzi utakaoamuliwa na wanafunzi wote.
Wanafunzi wakiwa wametawanyika mara baada ya mkutano huo kutawanyika na kufikia maamuzi ya kugoma.
Na Josephat Lukaza - University of Dodoma (UDOM)

Wanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma kitivo cha sayansi ya jamii, sanaa na lugha wamekusanyika mchana huu mbele ya bweni namba tatu na kwenye uwanja wa mpira wa kikapu kwaajili ya kumsikiliza raisi wa kitivo cha sayansi ya jamii Mh Mwakibinga Philipo Kwa ajili y kuelez jinsi ya serikali yake ilivyoweza kufanya yote yaliyowezekana kufanywa na serikali yake na kuwapa wanafunzi wenyewe waamue mara baada ya serikali nzima ya wanafunzi kufuatilia swala hili kwa ngazi husika na kuonekana kuwa hakuna uwezekano wa suluhu iliyoweza kupatika.

Raisi wa Kitivo Cha sayansi Ya jamii, sanaa na lugha Ametubia katiba ya serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma UDOSO kuwapa mamlaka wanafunzi ya kuamua mara baada ya bunge kushindwa kutoa maamuzi katiba ya UDOSO inasema mada yoyote ile inayoshindikana kupata suluhu ndani ya kikao cha bunge basi maamuzi yataammuliwa na wanafunzi Mamlaka hayo ya katiba yamewapa wanafunzi uwezo wa kuamua pale bunge linaposhindwa kufikia muafaka.

Wanafunzi Wamefikia Muafaka wa Kugoma hapo kesho Kuanzia Saa Kumi Alfajili Kwaajili ya kwenda bungeni kuonana na Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda Kwaajili ya Kuweza kupata uamuzi juu ya maswala mazima kuhusu mafunzo kwa vitendo kitu ambacho kiliahidiwa na Waziri wa Elimu Shukuru Kawambwa na Waziri Wa Mambo ya Ndani Mh Shamsi Vuai Nahodha Kuwaahidi wanafunzi wa kitivo hiki kuwa wataenda kufanya mafunzo kwa vitendo wakati walipofika kusuluhisha mgomo uliotokea tarehe 20 Disemba 2010 

Katika Usuluhishii huo Waziri Kawambwa Na Shamsi Vuai Nahodha Waliweza kuwaagiza uongozi wa chuo na Tume ya vyuo vikuu Tanzania pamoja na Bodi ya mikopo kufanya mchakato wa haraka kuwezesha wanafunzi ambao hawana mafunzo kwa vitendo wanakwend katika likizo ndefu ambayo inatakiwa kuanza mara baada ya wanafunzi kumaliza mitihani yao ya mwisho wa muhula inayomalizika tarehe mosi julai 2011
Mgomo Huu Mkubwa Ambao umeweza kuhusisha  baadhi yavyombo vya serikali umekuja mara baada ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania Kutoa Tangazo kuwa hakuna kwenda kufanya mafunzo kwa vitendo kwa kozi ambazo hazina mafunzo kwa vitendo, tangazo hilo limesababisha wanafunzi, uongozi wa chuo kushangaa uamuzi uliofikiwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania Kwa kutoa tangazo hilo wakati walikuaa wameshakubaliana na Waziri Wa Elimu tayari alishatoa maamuzi.

kwa muendelezo wa habari hizi 

No comments:

Powered by Blogger.