16/6/2011 Leo ni siku ya Mtoto wa Afrika
Serikali haishabikii vituo vya watoto wa mitaani
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto katika
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Bi Tukae Njiku ametoa msimamo
huo kwa niaba ya Waziri wa wizara hiyo jana jijini Dar Es Salaam wakati
akiongea na waandishi wa habari kuhusu kilele cha siku ya mtoto wa Afrika.
“Serikali haisisitizi kuweka watoto
kwenye vituo. Kufanya hivyo iwe ni hatua ya mwisho wakati unatafutwa ufumbuzi
wa tatizo la watoto wa mitaani,” amesema.
Katika mkutano huo ulioudhuriwa na
watendaji wengine wa wizara hiyo, Bibi Tukae ameeleza kuwa vituo vya watoto
yatima lazima viwesajili na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
“Kama kituo kipo, serikali itataka kujua kama kimesajiliwa, baada ya kujiridhisha kuwa kinafaa
kulelea watoto. Lakini kama kituo kinafanyakazi bila kusajiliwa, kituo hicho ni
batili na kinatakiwa kufungwa,” amesema.
Takwimu
zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) kwa
kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) zinaonyesha kuwa watoto wa
mitaani duniani wanakadiriwa kufikia milioni 120, milioni 30 kati ya hao wako
barani Afrika.Aidha utafiti
uliofanywa Shirika lisilo la kiserikali Consortium for Street Children mwaka
2009 yanayoonyesha kuwepo sababu mbalimbali zinazochangia kuongezeka kwa watoto
wa mitaani nchini.
Kwa mujibu wa utafiti huo, ukatili dhidi ya watoto unachangia
kuwepo kwa asilimia 50 za watoto wanaoishi mitaani, njaa na
umaskini 35%, ukosefu wa upendo 11% na kuvunjika kwa familia 4%.
Siku ya Mtoto wa Afrika uadhimishwa na
nchi zote wanachama wa Umoja wa Afrika kwa mujibu wa Azimio lililopitishwa na
Umoja huo mwaka 1990. hapa nchini kila mkoa utaadhimisha siku hii kwa
kushirikisha Halmashauri zake pamoja na tarafa, kata na vitongoji.
Kauli
mbiu ya mwaka huu ni
“Tuungane
kwa pamoja kuchukua hatua za haraka kushughulikia tatizo la watoto wanaoishi
mitaani.”
No comments:
Post a Comment