Header Ads

LAYD JD ATEMBELEA HOSPITALI YA CCBRT NA KUJIONEA WANAWAKE WANAOSUMBULIWA NA GONJWA HATARI LA FISTULA

Jide, Erwin Telemans ambae ni CEO wa CCBRT, na Brenda Msangi ambae ni Community Programmes Director mchana wa jumatano nilipo zuru Hospitalini hapo kutembelea wodi mbali mbali za wagonjwa

Mama ambae alikuwa na tatizo la ugonjwa wa Mdomo Sungura "Cleft Lip" yeye pamoja na watoto wake wote wawili, hapa ni mara baada tu ya kufanyiwa surgery ili kurekebisha tatizo hilo
Hospital hiyo yenye usafi na hadhi ya hali ya juu tofauti na Hospital zingine nchini inatoa matibabu ya mangonjwa ya aina mbali mbali ya ulemavu

Hii ni Wodi ya Fistula ambapo haswa ndio lilikuwa lengo langu kutembelea Hospitali ya CCBRT.
FISTULA ni ugonjwa hatari unaowapata wasichana na wanawake wakati wa kujifungua.Wasichana/Wanawake wanao ishi katika mazingira duni na ya kimaskini wanajikuta wanalazimika kujifungulia majumbani mwao wakisaidiwa na wakunga badala ya kwenda Clinic za Wazazi.
Jambo linalopelekea wanapatwa na ugumu wakati wa kujifungua na kusababisha kupatikana kwa ugonjwa wa Fistula.
Madhara ya Fistula ni msichana/mwanamke kupatwa na haja ndogo au haja kubwa bila kujijua na hali hii huwatokea mara kwa mara na hawawezi kujizuia.
Mwanamke alie na Fistula hulazimika kuacha kazi au kwa familia zisizo elewa hutokea pia kutengwa na watu wa karibu kutokana na kuwa na harufu ya kutokwa haja mara kwa mara hata mbele za watu bila kujijua.
Kwa wastani wasichana/wanawake milioni 2 Africa na Asia ya kusini wanaishi na Fistula.
FISTULA INATIBIKA
Na cha kufurahisha zaidi CCBRT inatoa matibabu ya ugonjwa huo bure.
Kama una mtu yoyote unamfahamu ana tatizo hili hata kama hana hela ya usafiri kutoka popote alipo, iwe mjini au kijijini hapa nchini Tanzania.
Tafadhali chukua jukumu la kuwasiliana na CCBRT au hata mimi ili tuweze kuokoa maisha ya mwanamke.
CCBRT iko tayari kumgharamia afike Hospital na atapata matibabu bure pamoja na huduma zote za msingi kama chakula na malazi.
Na akishapona pia atapatiwa usafiri wa kurudi popote alipotokea.

No comments:

Powered by Blogger.