Meneja
wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Singida Eng. Leonard
Kapongo (wa kwanza kushoto), akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto) kuhusu
mradi wa ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti linalounganisha Wilaya ya
Mkalama mkoani Singida na Meatu mkoani Simiyu.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili
kushoto) akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara nchini
(TANROADS), mkoa wa Singida Eng. Leonard Kapongo (wa kwanza kushoto)
kuhusu usimamizi wa ujenzi wa Daraja la mto Sibiti.
Muonekano
wa moja ya nguzo inayoshikilia Daraja la Mto Sibiti linalounganisha
Wilaya ya Mkalama mkoani Singida na Meatu mkoani Simiyu.
Mkuu
wa Wilaya ya Mkalama Bw. Christopher Ngubiagai (katikati), akifafanua
jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa
(wa kwanza kushoto) alipokagua ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza
kushoto) akikagua jengo la nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Mkalama
linalojengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA) mkoani Singida.
Muonekano
wa juu wa Daraja la Msingi lenye urefu wa mita 75 linalounganisha
Wilaya ya Mkalama na Iramba, lililopo mkoani Singida.
Muonekano
wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama inavyoonekana
katika hatua za awali za ujenzi wake. Zaidi ya milioni 758 zinatarajiwa
kutumika katika ujenzi huo.
Msimamizi
wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama (wa kwanza
kulia), akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto), kuhusu hatua za ujenzi wa
ofisi hizo mkoani Singida.
DARAJA LA MTO SIBITI KUKAMILIKA HIVI KARIBUNI; PROF. MBARAWA
Reviewed by
crispaseve
on
5:14 AM
Rating:
5
No comments:
Post a Comment