KABURI MOJA WALIMOZIKWA WATU 425 LAGUNDULIKA KINSHASA-DRC
Baadhi wananchi wanasema kuwa, mauaji dhidi ya watu hao yalitokea wakati wa machafuko ya mwezi Januari mwaka huu, huku wengine wakisema kuwa, mamia hao walifia hospitali.
Kaburi hilo limegunduliwa katika eneo la mji wa Maluka, katika viunga vya mji wa Kinshasa baada ya malalamiko ya wakazi wa eneo hilo kushindwa kuvumilia harufu kali iliyokuwa ikitokea eneo la kaburi hilo, hivyo kuamua kutoa taarifa kwa vyombo vya habari na serikali ya nchi hyo.
Baadhi ya duru zimethibitisha kuwa wahanga hao waliuawa katika machafuko ya tarehe 19-21 mwezi Januari, wakati wa maandamano ya kupinga njama za serikali kuifanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo kwa lengo la kumbakisha zaidi madarakani Rais Joseph Kabila.
Hata hivyo Evariste Boshab Mabudj, Waziri wa Mambo ya Ndani wa DRC alipotakiwa kuzungumzia suala hilo amekanusha madai hayo na kusema kuwa, wahanga hao walipoteza maisha kwa maradhi hospitalini.
No comments:
Post a Comment