Waziri Fenella akutana na wasanii nchini
Waziri
wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiongea
na wasanii nchini na kuwaasa wasanii kuielimisha na kuhamasisha Jamii
kuhusu Katiba Inayopendekezwa kupitia kazi mbalimbali za sanaa, wakati
wa mkutano na wasanii nchini uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri
wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara
akimueleza jambo Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt.
Francis Michael wakati wa mkutano na wasanii uliofanyika katika ukumbi
wa uwanja mpya wa Taifa leo Jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi
Idara ya Utamaduni kutoka Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo
Prof. Herman Mwansoko akiongea na wasanii nchini na kuwaeleza kuhusu
umuhimu wa sekta hiyo kushiriki kikamilifu katika masuala ya kitaifa
hasa katika kipindi hiki cha kuelekea upatikanaji wa Katiba Mpya, Kulia
ni Katibu wa Bodi ya Filamu Bi. Joyce Fisoo.
No comments:
Post a Comment