Header Ads

Viongozi wa Dini waaswa kuhubiri amani na utulivu kuelekea mchakato wa Katiba Mpya

DI1 
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Magharibi Bw.Ayoub Mohamed Mahmoud akiongea na Viongozi mbalimbali wa Dini na kuwataka kuhubiri amani na utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea upigaji kura ya maonikwa Katiba Inayopendekezwa pamoja uchaguzi Mkuu
DI3 
Mbunge wa WAWI kupitia chama cha wananchi CUF Mh. Hamad Rashid Mohamed akiongea na viongozi wa Dini mbalimbali na kuwaasa kuisoma, kuielewa Katiba Inayopendekezwa na kuacha kupotoshwa kwa kusomewa vipengele vya Katiba hiyo bila kupewa ufafanuzi, wakati wa mkutano ulioratibiwa na Kamati ya Amani na Utulivu Tanzania kushirikisha viongozi wa Dini leo Zanzibar.
DI4Mwenyekiti wa Kamati ya Amani na utulivu Tanzania Sheikh Noman Thabit Jongo akiwaeleza viongozi wa Dini mbalimbali suala la amani na utulivu katika kuelekea katika kuipigia kura ya maoni Katiba Inyopendekezwa na kuwaasa kuwaelimisha waumini wao juu ya ubora wa Katiba Inayopendekezwa kwani imegusa makundi yote katika Jamii
DI5 
Katibu wa Kamati ya Amani na utulivu Tanzania Padri. Damas Mfoi akiongea katika mkutano wa Kamati ya Amani na Viongozi wa Dini mbalimbali Zanzibar na kuwaasa kusambaza ujumbe wa Amani na kuepuka mambo yoyote yatakayoashiria uvunjifu wa amani hasa katika kipindi hiki Taifa likielekea katika Mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya na Uchaguzi Mkuu.
DI6 
Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa Dini Zanzibar wakifuatilia Mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika Mkutano huo
DI7 
Mmoja ya Mjumbe wa Mkutano akifanya rejea katika Katiba Inayopendekezwa wakati wa uwasilishwaji wa Mada katika Mkutano huo. (PICHA NA HASSAN SILAYO)

No comments:

Powered by Blogger.