MHE. LUKUVI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA NYUMBA MPYA ZA MAKAZI ZA NHC MJINI SUMBAWANGA, APOKEA MALALAMIKO MBALIMBALI YA MIGOGORO YA ARDHI KUTOKA KWA WANANCHI WA MKOA WA RUKWA

Waziri
wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wa tatu
kulia na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya wa kwanza kushoto
wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba 20 za makazi zinazojengwa na
Shirikia la Nyumba la Taifa (NHC) katikati ya Manispaa ya Sumbawanga
tarehe 26/03/2015. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Ndugu
Nehemia Mchechu nyumba hizo ambazo ni za ghorofa moja zitauzwa baada ya
kukamilika ujenzi wake kwa njia ya fedha taslimu na njia ya Mikopo ya
benki.

Waziri
wa Ardhi Mhe. William Lukuvi katikati akiweka jiwe la msingi mradi wa
ujenzi wa nyumba 20 za makazi zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa
Mjini Sumbawanga kwa kushirikiana na viongozi wengine wa chama na
Serikali Mkoani Rukwa tarehe 26/03/2015.
Waziri
wa Ardhi Mhe. William Lukuvi kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu
wa Shirika la Nyumba la Taifa Ndugu Nehemia Mchechu katika hafla fupi ya
uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa nyumba za makazi za shirika
hilo Mjini Sumbawanga.
Michoro ya mradi huo.
No comments:
Post a Comment