Header Ads

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAFANYA UKAGUZI KWENYE VITUO VYA KUPOOZA NA KUSAMBAZA UMEME KATIKA MIKOA YA ARUSHA NA KILIMANJARO


ka1
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum Jimbo la  Singida, Martha Mlata (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya  Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) Dkt. Miganda Manyahi (kulia), jijini Arusha kabla  ya kuanza kwa ziara kwenye miradi ya  umeme. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini  inafanya  ziara katika miradi ya umeme iliyopo katika mikoa  ya Arusha na Kilimanjaro ili  kujionea hatua  ya utekelezwaji wake pamoja na kuzungumza na watendaji.
ka2
Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini  Richard Ndassa  (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha,  Daudi Felix Ntibenda (kulia) mara baada ya Kamati  hiyo kuwasili ofisini  kwake kwa ajili ya kupokea taarifa ya mkoa kabla ya kuanza kwa ziara kwenye miradi ya umeme.
ka3
Mkuu wa Mkoa wa Arusha,  Daudi Felix Ntibenda ( wa nne kutoka kushoto waliosimama mbele), Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini  Richard Ndassa ( wa tano kutoka kushoto waliosimama mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kudumu  ya Bunge ya Nishati na Madini na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini mara baada ya kumalizika  kwa kikao.
ka4
Meneja Mradi wa  Kusambaza  Umeme unaojulikana kwa jina la  Electricity  V unaofadhiliwa na  Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Mhandisi  Florence Gwang’ombe
(kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini  Richard Ndassa (kulia) mara baada ya kamati hiyo kuwasili kwenye eneo la mradi huo ili kujionea maendeleo ya utekelezwaji wake.
ka5
Mtaalam kutoka Kampuni ya Sweco International AB,  Pal Aberg (kushoto) akiielezea Kamati ya Kudumu ya  Bunge ya Nishati na Madini  hatua iliyofikiwa ya  ujenzi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Njiro kilichopo nje kidogo ya jiji la Arusha.
ka6
Kamati ya Kudumu ya  Bunge ya Nishati na Madini  ikiendelea na ziara katika eneo la kituo cha kupooza na kusambaza umeme kilichopo Njiro nje kidogo ya jiji la Arusha.

No comments:

Powered by Blogger.