Header Ads

AMIN SALMINI AAHIDI KUIBORESHA OFISI YA SERIKALI YA MTAA KATA YA TABATA, WAKIFANYA SHEREHE YA KUWASHUKURU WAPIGA KURA WAO.

 Mtoto wa Rais Mstaafu wa awamu ya tano Zanzibar, Amin Salmin, akimkabidhi Cheti, Mwenyekiti wa UWT ambaye pia ni Kaimu Katibu wa CCM wa Tabata Relini, Shahani Mtwawa, wakati wa Sherehe maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwashukuru Wapiga Kura wa CCM, waliofanikisha kuchaguliwa kwa Viongozi wa Serikali ya Mtaa huo wa Kata ya Tabata. Sherehe hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika Ofisi za Serikali ya Mtaa Kata ya Tabata, jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake mgeni rasmi huyo, aliahidi kuiboresha Ofisi hiyo ya Serikali ya Mtaa wa Tabata kwa kununua Fenicha za ofisi zisizopungua gharama ya Sh. M 1.5. Picha na Sufianimafoto.com
 Mtoto wa Rais Mstaafu wa awamu ya tano Zanzibar, Amin Salmin, akisaini katika kitabu cha wageni, mara tu baada ya kuwasili kwenye ofisi hizo.
 Mtoto wa Rais Mstaafu wa awamu ya tano Zanzibar, Amin Salmin, akimkabidhi Vifaa vya michezo (Jezi na Mpira)  Katibu Mwenezi wa Kata ya Tabata Relini, Ramadhan Mazongera,  wakati wa Sherehe maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwashukuru Wapiga Kura wa CCM, waliofanikisha kuchaguliwa kwa Viongozi wa Serikali ya Mtaa huo wa Kata ya Tabata. Sherehe hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika Ofisi za Serikali ya Mtaa Kata ya Tabata, jijini Dar es Salaam.
 Mtoto wa Rais Mstaafu wa awamu ya tano Zanzibar, Amin Salmin, akimkabidhi Vifaa vya Michezo (Jezi na Mpira) Mwakilishi wa Tawi la CCM la Mti Mgandisho Tabata, Bakari Mpakala, wakati wa Sherehe maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwashukuru Wapiga Kura wa CCM, waliofanikisha kuchaguliwa kwa Viongozi wa Serikali ya Mtaa huo wa Kata ya Tabata. Sherehe hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika Ofisi za Serikali ya Mtaa Kata ya Tabata, jijini Dar es Salaam.
  Sehemu ya Kinamama waliojitokeza kwenye sherehe hiyo.

No comments:

Powered by Blogger.