MAKALA YA SHERIA: JIHADHARI, HAUTARURUHUSIWA KUFANYA TRANSFER AU KUPATA HATI IKIWA UNA MKATABA WA SERIKALI ZA MITAA.

Hapo awali niliandika namna sheria isivyowaruhusu viongozi wa serikali za
mitaa kuandaaa na kusimamia mauzo na manunuzi ya nyumba au viwanja.
Nikasema kitu hicho hakiruhusiwi katika sheria na wanaofanya hivyo hakika
wako katika makosa makubwa. Nikasisitiza kuwa wewe ambaye mkataba
wako umeandikiwa serikali za mitaa ujue wazi kuwa mkataba wako wa
manunuzi hauna hadhi kisheria. Huu ni ukweli ambao nitazidi kuusema ili
kuwaepusha watu na usumbufu na ili watu wasiendelee kuingia katika utapeli
huu. Ndio, huu ni utapeli na ni jinai. Ni sababu hizihizi zinazowaingiza watu
wasio na hatia kwenye migogoro ya ardhi na kuwapotezea hela zao.
1.HUWEZI KUFANYA TRANSFER UKIWA NA MKATABA WA SERIKALI ZA MITAA.
Kwa wale ambao waliwahi kufanyia mikataba yao ya manunuzi ya nyumba/viwanja serikali za mitaa halafu wakaamua kwenda ardhi kubadili jina watakuwa wamekutana na hiki kitu ninachoongelea hapa. Ikiwa ulifanya manunuzi ya ardhi na ukasimamiwa na serikali za mitaa basi ujue huwezi kubadilisha jina kutoka kwa aliyekuuzia kuingia jina lako. Na hapo ni vyote yaani hati au leseni ya makazi. Huwezi kabisa kubadilsha kimojawapo kati ya hivyo ikiwa mkataba wako ni wa serikali za mitaa.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA
1.HUWEZI KUFANYA TRANSFER UKIWA NA MKATABA WA SERIKALI ZA MITAA.
Kwa wale ambao waliwahi kufanyia mikataba yao ya manunuzi ya nyumba/viwanja serikali za mitaa halafu wakaamua kwenda ardhi kubadili jina watakuwa wamekutana na hiki kitu ninachoongelea hapa. Ikiwa ulifanya manunuzi ya ardhi na ukasimamiwa na serikali za mitaa basi ujue huwezi kubadilisha jina kutoka kwa aliyekuuzia kuingia jina lako. Na hapo ni vyote yaani hati au leseni ya makazi. Huwezi kabisa kubadilsha kimojawapo kati ya hivyo ikiwa mkataba wako ni wa serikali za mitaa.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA
No comments:
Post a Comment