Header Ads

WATANO WAJERUHIWA KWA RISASI KATIKA SHOO YA CHRIS BROWN HUKO MAREKANI

 Chris Brown
Watu watano wameripotiwa kupigwa risasi na kujeruhiwa mapema asubuhi ya leo(Jan.11) katika klabu ya usiku ya Fiesta iliyopo   San Jose, California nchini Marekani.
Tukio hilo lilitokea wakati mwanamuziki Chris Brown aki-perform jukwaani kibao chake cha Loyal katika party  iliyopewa jina la Capricorn Bash  ambayo ilikuwa mahsusi kwa ajili ya kuwapongeza watu waliozaliwa kati ya mwezi Dec.22 na Jan.19 ambapo staa huyo alikuwa mshereheshaji wa shughuli hiyo.
Mtandao wa San Jose Mercury umeripoti kwamba tukio hilo lilitokea majira ya 1:20 usiku kwenye barabara ya Monterey Kabla ya polisi wa doria kufika eneo la tukio na kukuta watu 4 wakiwa wamejeruhiwa vibaya, wakati wengine watano wakikimbizwa hospitali jirani.
 Chris Brown amewajulisha mashabiki wake kuwa yupo salama salimini baada ya kuandika ujumbe mfupi kwenye ukurasa wake wa Twitter leo.  ”I’m”, aliandika Brown.
Polisi wamewaweka kizuizini watu kadhaa waliohusika kwenye shambulio hilo huku hali za majeruhi zikitajwa kuendelea vizuri.  Tazama tukio lilivyotokea hapo chini

No comments:

Powered by Blogger.