Header Ads

TANZIA : MSUMBIJI WATANGAZA MAOMBOLEZO YA SIKU TATU

Pichani ni Rais wa sasa wa Msumbiji Armando Guebuza
Pichani ni Rais wa sasa wa Msumbiji Armando Guebuza
Serikali ya msumbiji imetangaza maombolezo ya siku tatu kufuatia vifo vya watu 69 waliokufa baada ya kunywa pombe ya kienyeji inayodaiwa kuwa na sumu ambayo ni nyongo ya mamba wakiwa katika msiba nchini humo.
Katika maombolezo hayo serikali hiyo imeamuru bendera zote nchini humo kupepea nusu mlingoti huku ikiahidi kuwapa tiba stahili waathirika wa pombe hiyo na kuwasaka watu waliohusika katika kuweka sumu kwenye pombe hiyo ingawa mmoja kati ya watu hao tayari amekufa.
Baadhi ya waathirika wa pombe hiyo iliyotengenezwa kwa mtama na mahindi na kuchanganywa na kinachosadikiwa kuwa ni sumu ya nyongo ya Mamba bado wamelazwa katika hospitali za nchi hiyo kwa ajili ya uangalizi wa afya zao sambamba na ,tiba.

No comments:

Powered by Blogger.