Header Ads

RAIS FRANNCOIS HOLLANDE WA UFARANSA AHUDHURIA MAZISHI YA WACHORA VIBONZO WA CHARLIE HEBDO

Franncois Holland Charlie Hebdo
Rais Franncois Holland akitoa heshima za mwisho mbele ya majeneza yenye miili ya mapolisi waliouwawa katika shambulio
Mazishi ya wachora vibonzo saba wa jarida la Charlie Hebdo waliouwawa wiki iliyopita, yamefanyika mjini Paris Ufaransa huku watu wengine waliouwawa katika duka nchini humo wakitajwa kuzikwa mjini Yerusalem.
Aidha katika mazishi ya polisi waliouwawa katika mashambulizi hayo yamefanyika maziko ya heshima ambayo pia yamehudhuriwa na Rais Franncois Hollande.
Wiki iliyopita Ufaransa iligubikwa na mshtuko na taharuki kwa siku tatu wakati ndugu wawili waliposhambulia jarida la Charlie Hebdo kutokana na hasira kwamba jarida hilo limekuwa likikejeli dini ya kiislamu.
Rais  Franncois Holland
Rais Franncois Holland wa Ufaransa akipigiwa saluti na maafisa polisi nchini humo wakati alipohudhuriwa mazishi ya polisi waliouwawa katika shambulio

Cherlie Hebdo
Majeneza yenye miili ya waandishi habari wa jarida la Charlie Hebdo ambayo imetajwa kuzikwa mjini Yerusalem
Charlie Hebdo
Waombolezaji wakiwa na nyuso za huzuni

No comments:

Powered by Blogger.