MAZIKO YA MSHAURI WA RAIS UTALII YAFANYIKA ZANZIBAR
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa tatu kulia) Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Amani Abeid Karume (kulia) na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Viongozi wengine na waislamu mbali mbali wakijumuika kwa pamoja kumswalia aliyekuwa Mshauri wa Rais wa Utalii Marehemu Issa Ahmed Othman katika Masjid Mahfoudh Mazizini, Marehemu alifariki juzi Nchini India na kuzikwa leo Kianga Wilaya ya Magharibi Unguja.
Baadhi
ya Vijana na wananchi waliobeba Jeneza la Marehemu Issa Ahmed Othman
aliyekuwa Mashauri wa Rais Utalii Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
wakiupeleka kuzikwa kijijini Kianga Wilaya ya magharibi Unguja leo
jioni,marehemu alifariki juzi Nchini India ambako alikwenda kwa
matibabu,[Picha na Ikulu.]
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Balozi Seif Ali Iddi
(katikati) pamoja na Viongozi wengine na waislamu mbali mbali
wakijumuika kwa pamoja katika mazishi ya aliyekuwa Mshauri wa Rais wa
Utalii Marehemu Issa Ahmed Othman katika Kijiji cha Kianga Wilaya ya
Magharibi Unguja leo jioni,[Picha na Ikulu.]
No comments:
Post a Comment