Header Ads

Waziri wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Nyalandu,ametangaza rasmi nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu 2015

 Waziri Nyalandu akiwa na watoto wake wakati wa ibada maalum iliyofanyilka leo katika Kanisa la KKKT Usharika wa Ilongelo Jimbo la Singida Kaskazini
 Nyalandu na Faraja Kota wakiwa na watoto wao Sera na Christopher katika kanisa hilo
 Mwimbaji wa nyimbo za Injili lkatika Kanisa la KKKT Usharika wa Ilongelo
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro  Nyalandu akitoa neno la shukrani baada ya ibada maalum katika katisa la KKKT Usharika wa Ilongelo jimboni humo leo
 Waumini wakiwa katika kanisa la FPCT wakati wa ibada maalum aliyohudhuria Nyalandu leo
  Nyalandu na Mkewe wakitoka katika Kanisa la FPCT baada ya kuhudhuria ibada maalum leo asubuhi. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu akizungumza na viongozi wa shule ya Kiislam ambayo huhudumia watoto wa dini zote katika kata ya Ilongelo, shule hiyo ina watoto 74.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akisalimia waumini kwenye Kanisa la FPCT  katika jimbo la Ilongelo alipofika kwa ajili ya ibada maalum
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazalo Nyalandu alisalimia wananachi baada ya kuwasili na mkewe Faraja Kota kwenye Mkutano wa jimbo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo, jimboni humo
   Steve Nyerere ambaye ni Msanii na Kamanda wa Umoja wa Vijana wa CCM, akizungumza kabla ya kumwaga vimbwanga vyake vya kuingiza sauti za viongozi mbalimbali wakati wa mkutano huo wa Nyalandu.
   Mwimbaji wa muziki wa Injili, Frola Nkone akiimba kutumbuiza wakati wa mkutano huo

 Mwanamuziki wa muizki wa Injili, Rose Mhando akiimba kutumbuiza wananchi katika mkutano huo wa Nyalandu
  Wadau wakifurahia burudani wakati wa mkutano huo wa Nyalandu
 
 Wasanii wa kikundi cha Makomandoo cha mjini Singida wakitumuiza wakati wa mkutano huo
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazalo Nyalandu alisalimia wananachi baada ya kuwasili na mkewe Faraja Kota kwenye Mkutano wa jimbo uliofanyika leo kwenye Uwanja wa Michezo wa Ilongelo, jimboni humo.Picha na Bashir Nkromo
----
WAZIRI wa maliasili na utalii na mbunge wa jimbo la Singida kaskazini(CCM) ,Lazaro Samwel Nyalandu,ametangaza rasmi nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani. 

Nyalandu ametangaza nia hiyo leo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Ilongero Jimbo la Singida kaskazini.

No comments:

Powered by Blogger.