Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi,Profesa Anna Tibajuka Akutana na Waandishi wa Habari Jijini Dar na Kutoa Msimamo Wake Kwamba Hana Sababu ya Kujiuzuru Kwenye Nafasi Yake Kwa Kuwa Hakuhusika Kwa Namna Yeyote Kwenye Sakata la Uchotwaji wa Mabilioni Kwenye Akaunti ya Escrow.

Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Makazi,Profesa Anna Tibajuka akizungumza na
Waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye ukumbi wa mikutano kwenye
hoteli ya Hyatt Regency,Jijini Dar es salaam leo.

Sehemu
ya Waandishi wa Habari waliofika kwenye Mkutano huo ulioitishwa na
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi,Profesa Anna Tibajuka.

Sehemu ya Umati wa Waandishi wa Habari.Picha na Chalila Kibuda-Globu ya Jamii
Siku Moja baada ya kujiuzuri kwa Mwanasheria mkuu Jaji Fredrick
Werema, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna
Tibaijuka kwa mara nyingine amejitokeza hadharani na kutoa msimamo wake
kwamba hana sababu ya kujiuzuru kwenye nafasi yake kwa kuwa hakuhusika
kwa namna yeyote kwenye sakata la uchotwaji wa mabilioni kwenye akaunti
ya Escrow.
Akizungumza na waandishi wa habari asubuhi jijini
Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa
shinikizo la kutaka kujiuzuru, yeye binafsi ameona hana sababu ya
kufanya hivyo kwani kufanya hivyo ni kukubali kuwa amehusika moja kwa
moja kwenye kashfa hiyo jambo ambalo si la kweli.
No comments:
Post a Comment