Mwenyekiti mweza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Dk Emmanuel Makaidi amejitolea kusuluhisha mgogoro baina ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na chama chake cha Chadema.

Mwenyekiti
wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Kigoma Kaskazini -Chadema Zitto
Kabwe walipokua wakiondoka katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es
Salaam baada ya kuwasilisha maoni ya chama hicho juu ya uundwaji wa
Katiba Mpya, kwa viongozi wa tume ya kukusanya maoni hayo,Mapema Mwaka
Huu. Picha
Salhim Shao
Mwenyekiti mweza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Dk Emmanuel Makaidi
-----
Mwenyekiti mweza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Dk
Emmanuel Makaidi amejitolea kusuluhisha mgogoro baina ya Mbunge wa
Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na chama chake cha Chadema.
Hatua ya mwanasiasa hiyo mkongwe ambaye pia ni
Mwenyekiti wa NLD, imekuja siku chache baada ya kuibuka hoja mbalimbali
katika mitandao ya kijamii zikishawishi Zitto kurejea Chadema hasa baada
ya kauli yake bungeni kuwa amekuwa akiwakosa wanasiasa wenzake wa
upinzani wanaounda kundi la Ukawa.
Ijumaa wiki iliyopita, Zitto alikaririwa na gazeti
hili akisema yuko tayari kurudi Chadema kwa sharti kwamba mgororo baina
yao ujadiliwe kwa uwazi na upande wenye makosa uombe radhi kwa uwazi
pia, huku Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akisema suala hilo lina
njia zake na siyo la kuzungumza katika vyombo vya habari.
No comments:
Post a Comment