MHESHIMIWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AMUWAKILISHA RAIS JAKAYA KIKWETE KWENYE MKUTANO WA MAZINGIRA (COP20) JIJINI LIMA, PERU DESEMBA 10, 2014

Katibu Mkuu, Ban Ki-Moon, akizungumza katika mkutano huo........

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia katika Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya
Tabianchi, unaoendelea Jijini Lima nchini Peru. Makamu wa Rais
alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio
mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na mambo mengine Dkt.
Bilal alizungumzia namna nchi za Afrika zilivyojizatiti katika maazimio
mbalimbali yanayolenga kunusuru majanga yatokanayo na Tabianchi.

Ujumbe wa Tanzania, katika mkutano huo.....

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akipiga picha ya kumbukumbu na Mkuu wa Ujumbe wa China, katika mkutano
wa Mkutano wa 20 wa Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Xie
Zhenhua, wakati walipokutana kwa mazungumzo baada ya kuhudhuria na
kuhutubia katika mkutano huo unaoendelea Jijini Lima nchini Peru, ambapo
alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu utekelezaji wa maazimio
mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akizungumza na Mjumbe maalum wa Marekani katika masuala ya Mabadiliko
ya Tabianchi, Todd Stern, baada ya kuhudhuria katika Mkutano wa 20 wa
Kimataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, unaoendelea Jijini Lima nchini
Peru, ambapo alizungumza kwa niaba ya nchi za Afrika kuhusu
utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi.

Makamu wa Rais na ujumbe wake .......

Makamu
wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiongozana na baadhi ya Mawaziri wakati wakitoka katika chumba cha
mkutano huo

Taswira ya kumbi za mikutano hiyo.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
----
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
jana Desemba 09, 2014 amemuwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye
ni Mwenyekiti Kamati ya Wakuu wa Nchi na Serikali Barani Afrika kuhusu
Mabadiliko ya Tabia Nchi, kwenye mkutano wa Kimataifa wa Mazingira
Duniani (Cop20) unaofanyika jijini Lima, Peru.
No comments:
Post a Comment