Header Ads

REBECA MALOPE AWAKUNA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA,NGELEJA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KULIOMBEA TAIFA


Pichani kati Mgeni rasmi,Mh.William Ngelleja akizindua albamu mpya ya nyimbo za injili ya muimbaji Grace Mwikwabe (pichani shoto) na kulia ni Mkurugrenzi wa Msama Promotions ambao ndio waandaji wa matamasha hayo ya pasaka na Xmass.
Mgeni rasmi katika muendelezo wa tamasha la Pasaka,ambaye ni Mbunge wa jimbo la Sengerema,Mh.William Ngereja akizungumza machache mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa jiji la Mwanza waliojitokeza kwenye tamasha hilo,Ngeleja aliwataka viongozi mbalimbali kuliombea Taifa wakati likipita katika kipindi hiki kigumu cha mchakato wa kuipata Katiba, na pia aliwataka Wananchi nchini Kote kuwa watulivu,kwani Mungu ni mwema mchakato wa kuipta katiba mpya utakwisha tu katiba mpya itapatikana.
Mkurugenzi wa Msama Promotions,Alex Msama akitoa neno la Shukurani kwa viongozi wa dini mbalimbali pamoja na wakazi wa jiji hilo waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la mwendelezo wa Pasaka,lililofanyika ndani ya uwanja wa CCM Kirumba hapo jana,Wakati huo huo katika tamasha hilo mgeni rasmi alikuwa ni Mh.William Ngeleja.
Mwanamuziki Rebecca Malope na skwadi lake zima wakiimba jukwaani ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza hapo jana.
Rebecca Malope akiimba kwa hisia jukwaani

 Mambo ya Facebook na Twitter hayo live
Mwimbaji nyota wa nyimbo za kiroho kutoka nchini Afrika Kusini,Rebecca Malope akitumbuiza jana jioni katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza,ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa tamasha la Pasaka huku likiwa limebeba kauli mbiu maridhawa kabisa isemayo Tanzania Kwanza,Haki Huinua Taifa.
Sehemu ya umatii wa watu wakifuatilia tamasha hilo.
Mwimbaji nyota wa injili hapa nchini Rose Muhando akiwaimbisha washabiki na wapenzi wa nyimbo za injili ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza hapo jana wakati wa mwendelezo wa tamasha la pasaka,ambalo limepokelewa vyema na wakazi wa jiji hilo.
Wadau wakiwa kwenye mashine zao wakihakikisha kila kitu kinakwenda sawa kwenye tamasha hilo ambalo lilipokelewa vyema na wakazi wa jiji la Mwanza.
Waimbaji mbalimbali mahiri wakishambulia jukwaa kwa pamoja ndani ya uwanja wa CCM Kirumba hapo jana wakati wa mwendelezo wa tamasha la pasaka jijini Mwanza
Mkurugenzi wa Msama Promotions,Alex Msama akimuongoza mwanamuziki mahiri wa nyimbo za injili kutoka nchini Afrika Kusini,Rebecca Malope mara baada ya kumaliza kutumbuiza ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza,Malope alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzikonga nyoyo za washabiki wa jiji hilo vilivyo.
Pichani ni sehemu ya umati wa watu wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza hapo jana wakati wa mwendelezo wa tamasha la Pasaka.
Mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka nchini Kenya,Sara K akiimba kwa hisia mbele ya wakazi wa jiji la Mwanza waliolipokea vyema tamasha hilo la mwendelezo wa pasaka.
Sehemu ya umati wa watu wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ndani ya uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili,Grace Mwikwambe akiimba

No comments:

Powered by Blogger.